MAREHEMU SHIRLEY MAGARI AZIKWA MOROGORO.



 Rais wa shilikisho la filam nchini'Bongo Movie' Simon Mwakifambo (wapili  kushoto mwenye full Jins) akiwa nje ya kanisa na baadhi ya sanii wa filam nchini
 Wasanii Jasmini Emiry [kulia] Asha Boko[kati] na mke wa mzee Mjuto Rehema Majutoa wakiwa kwenye ibada ya kumuombea marehemu Sherry iliyofanyika jana jioni katika kanisani kuu la Mtakatifu Patriki Morogoro. 
 Bi,Flora Msiba ambaye ni askali polisi kituo kikuu cha polisi Morogoro akiaga kwa uchungu mwili wa mepndwa mtoto wake wa kwanza Sherry
 Afande Flora akimpiga busu la mwisho mtoto wake huyo kipenzi
 Kiongozi wa Bongo Movie mkoa wa Morogoro Babuu akimsaidi Lidya kati kumuaga dada yake mpendwa.
 Mdogo huyo wa marehemu aliamua kurejea kwa mara ya pili kumuaga dada yake
 Msanii Tausi akimuaga msanii mwenzake  kwa uchungu
         Tausi akizidi kumlilia Sherry
 Tausi akisaidi kutoka kanisani baada ya kuaga

 Msanii Tunu Mgoranzi akiangua kilio kwa uchungu
 Msanii Tunu akitoka kanisani na pacha wake baada ya kuaga
 Shosti mkubwa wa marehemu Sherry msanii Mahinda akiangua kilio baada ya kuaga mwili wa rafiki yake kipenzi
 Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie  mkoani Morogoro wakishiriki kwenye ibada hiyo
 Umati wawatu uliofulika kanisani hapo
 Mwili wa marehemu Sherry ukitolewa kanisani baada ya lbada kumuombea kukamilika
 Afande Flora akisaidiwa kutoka kanisani 
 Mwili wa Sherry ukipakiwa kwenye gari tayari kwa safari ya kueleka  kwenye nyumba yake ya milele makabuli ya Kolla 


 Rais wa bongo Movie akiwaongoza waombolezaji kueleka makabuli ya Kola
          Marehemu Sherry enzi za Uhai wake.


Na Dustan Shekidele,Morogoro.
MSIBA wa msanii Sherry Choka,maarufu Sherry Magali umetawaliwa na vituko kibao,baba mzazi mzee Salim Choka na baba wa hiyari mzee Charles Magali waingia mitini mziba wa mtoto wao Mama mzazi Afande Flora Msiba awatosa wazazi hao na kuamuakuandika jina la baba yake Mzee Msiba Edward kwenye Msalaba wa mpendwa mtoto wake. 

Kama kawa baada ya vituko hivyo Mwandishi wa mtandao huu alimtafuta msemaji wa familia hiyo Kulwa Choka ambapo alikiri kuwepo kwa vituko hivyo.

” Nikweli baba yetu mzee Choka yuko Tunduma hakuweza kufika kwenye msiba wa mwanae na kwamba amepiga simu nakumpa madalaka yote babu yetu mzee Msafiri Ngedele ndio maana unaona msiba uko hapa  Mji Mpya nyumbani kwa mzee huyo, pia huyo mzee Magali ambaye watu wanadai ni baba yake Sherry pia hakufika msibani"alisema Kulwa kwa Jazba na kuongeza kusema

"kuhusu jina la kwenye msalaba tumekuwa na mvutano wa takribani masaa 4 kwenye kikao mama wa marehemu alitushangaza kuacha jina la baba wa marehemu mzee Choka na kung’ang’ania kuandika msalaba jina la baba yake mzee Msiba  Edward ambaye ni babu wa dada yangu sherry kwa upande wa mama yake,tumeona tusiwape watu faida tumekubali lakini undani zaidi wa matukio hayo tutakujuza baada ya kumaliza msiba huu”alisema Kubwa Choka ambaye amechangia baba na marehemu Sherry. 

Juhudi za Mtandao huu za kutaka kuzungumza na Mama mzazi wa Sherry Afande Flora Msiba zilikwama baada ya mama huyo muda wote kuangulia kilio kwa kuondokewa na mpendwa mtoto wake juhuzi hizo zinaendele leo na kesho,Pia juhuzi za Mwandishi wetu kumhoji mzee Choka kwa njia ya simu zinaendele, 

Pekuapekua ya Mtandao huu imefanikiwakumbana mmoja wa wasanii nyota wa bongo Movie kutoka Dar ambapo alipoulizwa kwa nini mzee Mgali hakufika kwenye msiba wa Sherry alisema” Nikweli mzee magari hakufika kwenye msiba wa Sherry yuko Mwanza kwenye shughuli za kisanii”alisema msanii huyo  aliyeomba hifadhi ya jina lake.

Picha na habair kwa hisani ya Shekidele Blog

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA