- Get link
- Other Apps
Watu wanne wanashikiliwa na polisi mkoani Kigoma kwa tuhuma za kuchoma moto ofisi ya masijala ya Idara ya Ardhi ya Manispaa ya Kigoma Ujiji na kuteketeza hati na nyaraka mbalimbali.
Alisema Oktoba mosi, mwaka huu saa 4.15 usiku, ofisi ya masijala ya idara hiyo ilichomwa moto na kuteketeza hati na nyaraka mbalimbali. Kamanda Ibrahim alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kitendo hicho ni njama za kupoteza vielelezo nyeti.
Alisema kuwa uchunguzi umebaini kuwa idara hiyo imegubikwa na migogoro inayohusiana na ugawaji wa viwanja.
“Uchunguzi wetu wa awali unaonyesha watu hao walitumia mafuta ya petroli kuchoma ofisi hiyo…tunaendelea kufuatilia zaidi tukio hili,” alisema Ibrahim.
Comments