SSRA yajipanga kuboresha Sekta ya Hifadhi ya Jamii.

       

Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bi. Irene Isaka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu  hatua zilizochukuliwa na mamlaka hiyo katika kuboresha sekta ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini. Kushoto ni Mkuu wa  Mahusiano na Uhamasishaji wa SSRA Bi. Sarah Kibonde Msika.
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bw. Ngabo Ibrahimu(Katikati)akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu maboresho ya Sheria ya Hifadhi ya Jamii na Miongozo iliyotolewa na Mamlaka hiyo inayolenga kuboresha sekta ya Hifadhi ya Jamii.Kushoto ni Mkuu wa Mahusiano na Uhamasishaji Bi. Sarah Kibonde Msika na Kulia ni Mkurugenzi wa Usajili na Matekelezo wa SSRA Bi. Lightness Mauki.
Mkuu wa Mahusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bi. Sarah Kibonde Msika akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu Mikakati ya Mamlaka hiyo katika kutetea na kulinda maslahi ya wanachama ikiwemo kuboresha Kikokotoo cha Mafao ya Pensheni.Kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kutoka SSRA Bw. Ngabo Ibrahimu.
Baadhi ya waaandishi wa habari wakiwasikiliza wawasilishaji kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) wakati wa Mkutano uliofanyika leo kwenye Ofisi za Mamlaka hiyo Jijini Dar Es Salaam.
Picha na Fatma Salum

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI