Emmanuel
Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ akiwa mbele ya usafiri na mjengo wake.
UTAJIRI wa komediani maarufu Bongo, Emmanuel Mgaya ‘Masanja
Mkandamizaji’ ni kufuru! Tena unatisha na sasa anaonekana kuwa miongoni
mwa wasanii wanaomiliki fedha na mali nyingi Bongo, Risasi Mchanganyiko
linakupa zaidi. HABARI MEZANI Awali, habari kuhusu utajiri wa Masanja
ilitua mezani mwa gazeti hili kama kidokezo, hapo mwandishi wetu
akaingia mzigoni na kuanza kuchunguza kwa kina mali anazomiliki msanii
huyo na kugundua kuwa ni kati ya mastaa mabilionea Bongo. “Masanja sio
yule tena.
Ana
mpunga (fedha) mrefu sana. Hakuna msanii wa maigizo Bongo anayeweza
kumfikia kwa sasa. Hao wengine ni mbwembwe tu, lakini pesa imelala kwa
Masanja,” kilipasha chanzo chetu. Kikaongeza: “Kwanza ana ghorofa lipo
Tabata, hapo ndipo anapoishi. Pia ana magari kibao ya kifahari, mashamba
ya mpunga na Kampuni ya OK Security inayolinda sehemu mbalimbali
zikiwemo taasisi nyeti nchini
Comments