Mh. Ummy Mwalimu afanya ziara ya kikazi Wilaya za Mkinga na Pangani


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu mwishoni mwa wiki amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Mkinga na Pangani kuhimiza wanawake kujiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuunga mkono juhudi za Serikali katika ujenzi wa Maabara.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mh. Ummy Mwalimu akikabidhi kadi ya (UWT) kwa Bi. Halima Kassim mmoja wa wanachama wapya katika Kata ya Maramba, Wilaya ya Mkinga.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mh. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wapya wa UWT mara baada ya kuwakabidhi kadi zao. Waliosimama kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mkinga, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi. Mboni Mgaza na Mbunge wa Viti Maalumu Al-Shymaa Kwegyir.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mh. Ummy Mwalimu (Wa nne kutoka kulia) akipata maelezo ya ujenzi wa maabara kutoka kwa Mwalimu Cyprian Taabani kutoka Shule ya Sekondari Daluni, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Daluni Mwanakombo Gobeto.
Mh. Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga akikabidhi bati (50) kwa Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi. Hafsa Mtasiwa ikiwa ni jitihada za kuunga mkono ujenzi wa maabara.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI