NI
balaa juu ya balaa! Miss Tanzania mpya wa mwaka 2014 aliyepokea taji
kutoka kwa Sitti Abbas Mtemvu, Lilian Deuce Kamazima, amejikuta akimwaga
chozi kufuatia kuanza kusakamwa kwa madai kwamba ni raia wa nchi
jirani ya Rwanda kwa kuzaliwa wazazi wake.
Miss Tanzania mpya wa mwaka 2014 aliyepokea taji kutoka kwa Sitti Abbas Mtemvu, Lilian Deuce Kamazima.
Hali
hiyo ilimpata juzikati aliposakwa na paparazi wetu aliyetaka ufafanuzi
kutoka kwake kwamba hata yeye hana sifa ya kuwa Miss Tanzania 2014 kwa
vile si raia wa Tanzania, achilia mbali Sitti aliyedaiwa kudanganya
umri.
Comments