- Get link
- Other Apps
Kanusho Kutoka Ofisi ya Mbunge na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa Kuhusu Uvumi Uliozagaa Kwenye Mitandao Mbalimbali ya Kijamii Kuwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa Kulazwa nchini Ujerumani
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mhe Edward Lowassa
Msemaji wa Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa,
Bw. Aboubakary Liongo
----
Ofisi ya
mbunge na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, jana ilikanusha vikali
uvumi uliozagaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa mbunge huyo
wa Monduli amelazwa nchini Ujerumani.
Taarifa zilizoenea zinaeleza kuwa Lowassa, ambaye wakati wote wa Mkutano wa 15/16 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano uliofanyika kwa wiki tatu, hakuwepo bungeni, amekuwa Ujerumani ambako amelazwa kwa matibabu.
Hata hivyo, jana msemaji wake, Aboubakary Liongo aliliambia gazeti hili kuwa taarifa hizo ni za uzushi lakini akaeleza ni kweli yuko nchini humo kwa ajili uangalizi wa afya yake.
Taarifa zilizoenea zinaeleza kuwa Lowassa, ambaye wakati wote wa Mkutano wa 15/16 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano uliofanyika kwa wiki tatu, hakuwepo bungeni, amekuwa Ujerumani ambako amelazwa kwa matibabu.
Hata hivyo, jana msemaji wake, Aboubakary Liongo aliliambia gazeti hili kuwa taarifa hizo ni za uzushi lakini akaeleza ni kweli yuko nchini humo kwa ajili uangalizi wa afya yake.
“Aliondoka kwenda India kumuona (mbunge wa Kilindi) Beatrice Shelukindo ambaye amelazwa huko na baada ya hapo alimpeleka mke wake Ujerumani kwa ajili ya kutibiwa matatizo ya miguu,”
“Alipofika huko na yeye akaamua kuangalia afya yake kwa kuwa daktari wake yuko nchini humo.” alisema Liongo.
Alisema
Lowassa atarejea nchini wiki ijayo kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za
sikuku ya Uhuru itakayofanyika Desemba 9 na baadaye ataelekea Monduli
kwa ajili ya kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika
Desemba 14.“Atakwenda kuhakikisha chama kinashinda nafasi zote katika uchaguzi huo,” alisema Liongo.
Comments