Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demoikrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Bara, Profesa Abdalla Safari na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar,
Salum Mwalimu wakiwa kwenye mazungumzo na Makamu wa Rais wa Bunge la
Ulaya (EP), Rainer Wieland, wakati ujumbe wa CHADEMA ulipofika Ofisi za
EP kuanza ziara ya kikazi kufuatia mwaliko wa bunge hilo.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Bara, Profesa Safari Abdalla akisalimiana na Makamu wa Rais wa Bunge la
Ulaya (EP) Rainer Wieland wakati ujumbe wa CHADEMA ulioko nchini
Ubelgiji, ulipofika ofisi za bunge hilo mjini Brussels kwa ajili ya
ziara ya kikazi. Wengine kutoka kulia ni Mwenyekiti wa BAVICHA, Patrobas
Katambi, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Katibu Mkuu wa
BAWACHA, Grace Tendega na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri John Mrema.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Bara, Profesa Abdalla Jumbe Safari akiwa na Makamu wa Rais wa Bunge la
Ulaya (EP), Rainer Wieland, walipokutana jana mjini Brussels, Ubelgiji
kwa mazungumzo, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya ujumbe wa CHADEMA
kufuatia mwaliko wa bunge hilo.
Comments