Baada
ya kuhutubia mkutano wa kampeni kwenye Kata ya Mwenge huko Lindi Mjini
Mama Salma Kikwete anaonekana akimbeba mtoto Juma Selemani ambaye naye
alikuwa miongoni mwa watu waliohudhuria mkutano wa kampeni.
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM anayewakilisha wilaya ya Lindi Mjini na Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia viongozi wa Chama Cha Mapinduzi
wa Kata ya Mtandi katika mkutano uliofanyika katika Mtaa wa Maisara kwa
ajili ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa nchini unaotarajiwa
kufanyika tarehe 14.12.2014.
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM anayewakilisha wilaya ya Lindi Mjini na Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia viongozi wa Chama Cha Mapinduzi
wa Kata ya Mtandi katika mkutano uliofanyika katika Mtaa wa Maisara kwa
ajili ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa nchini unaotarajiwa
kufanyika tarehe 14.12.2014.
Mama
Salma Kikwete, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi
anayewakilisha Lindi Mjini akishiriki kucheza na baadaye kuwahutubia
wananchi wa Kata ya Mwenge huko Lindi Mjini wakati akishiriki kuwapigia
kampeni za uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unaotarajiwa
kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014.
Mke
wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, CCM,
anayewakilisha Lindi Mjini, Mama Salma Kikwete akisalimiana na viongozi
wa Kata ya Mtandi iliyoko Lindi Mjini wakati alipotembelea Kata hiyo kwa
ajili ya kufanya mkutano wa kampeni katika uchaguzi wa viongozi wa
serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014.
Mama
Salma Kikwete, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi
anayewakilisha Lindi Mjini akishiriki kucheza na baadaye kuwahutubia
wananchi wa Kata ya Mwenge huko Lindi Mjini wakati akishiriki kuwapigia
kampeni za uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unaotarajiwa
kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014.John Lukuwi
----
Na Anna Nkinda – Lindi
Wanachama
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Lindi mjini wametakiwa
kutokubali kurubuniwa kwa kitu chochote kile ili wawapigie kura wagombea
wa vyama vya upinzani bali waungane kwa pamoja katika kampeni na
kuhakikisha chama hicho kinapata ushindi wa kishindo.
Mwito
huo umetolewa jana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM
kupitia wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete wakati akiwanadi kwa
wananchi wagombea wa chama hicho wanaowania nafasi za uongozi kwenye
uchaguzi wa Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za Mitaa katika Kata ya
Mwenge.
Mama
Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema lengo
la chama chochote cha Siasa ni kushika Dola kuanzia ngazi ya mtaa hadi
Taifa hivyo basi wanachama hao wasikubali kurubuniwa bali waendelee
kukitetea na kukipigania Chama chao ili kipate ushindi katika mitaa
yote 117 ya Kata hiyo.
“Viongozi
wanaogombea tena wamechaguliwa kutokana na kazi yao nzuri. Nanyi ambao
kura zeu hazikutosha wakati wa mchakato wa kuchagua msilaumu, bali
muwapiganie wagombea wote na kuhakikisha wanashinda angalieni maslahi
ya chama kwanza mambo binafsi baadaye”, alisema Mama Kikwete.
Aidha
Mama Kikwete aliwaomba wananchi wa wilaya hiyo kutumia maarifa na ujuzi
waliopewa na Mwenyezi Mungu wa kutambua mema na mabaya na kutokubali
kudanganywa na kundi la watu wachache ili waipoteze amani yao.
Mama
Kikwete alisema, “Wenzenu wamepiga hatua kubwa za maendeleo katika
mikoa yao huku Lindi Mwenyezi Mungu katupa neema maendeleo yanakuja
sasa. Wanakuja huku kuwadanganya ili mfanye vurugu na kurudisha
maendeleo yenu nyumba, msifuate mkumbo na kuchezea amani kwani vurugu
zinarudisha nyuma maendeleo”.
Aliwasihi
wananchi waliohudhuria mkutano huo kuhakikisha watoto wao wanaenda
shule ili wapate viongozi wazuri wa baadaye ambao watawaletea maendeleo
kwani bila ya kuwa na elimu ni vigumu kupata maendeleo.
MNEC
huyo pia aliwashukuru wanaume waliowaruhusu wake zao kugombea nafasi
mbalimbali za uongozi na kuwapongeza wanawake kwa kutokukubali kubaki
nyuma na kuomba kugombea nafasi hizo.
Mama
Kikwete yupo wilayani humo kwa ajili ya shughuli za kichama ikiwa ni
pamoja na kushiriki kwenye kampeni na kuwanadi wagombea wa chama hicho
wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa viongozi wa
Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji utakaofanyika tarehe 14 mwezi
huu.
Comments