Na Woinde Shizza,Arusha

Chama cha mapinduzi kimeibuka kidedea katika uchaguzi wa uwenyekiti wa mitaa katika mitaa yote iliopo ndani ya mkoa wa Arusha baada ya kuvishinda vyama vingine vya upinzani .

Akitangaza  matokeo ya uwenyeviti wa mitaa Mkurugenzi wa jiji la Arusha Iddi Juma alisema kuwa mpaka sasa uchaguzi wa uwenyekiti umekamilika katika mitaa yote na vituo vyote isipokuwa kituo kimoja ambacho uchaguzi wake utarudiwa siku ya kesho.

Alisema kuwa   katika uchaguzi huu jumla ya wananchi  1,13909 walijiandikisha kupiga kura na jumla ya vyama sita vilisimamisha wagombea katika kila mtaa ambapo alitaja vyama ambavyo vilisimamisha wagombea kuwa ni pamoja na ACT,chama cha mapinduzi CCM,NCCR mageuzi ,CUF pamoja na TLP   .

Akitaja matokeo ya uwenyekiti wa mitaa alisema kuwa ccm imeweza kuongoza kwa kupata mitaa mingi zaidi ambapo alisema kuwa CCM imeweza kupata kura 78 ambapo kati ya kura hizo kura sita ni za kupita bila kupigwa, ikifuatiwa na chadema ambao wana kura 75 ,ACT ikiwa aijapata kura ,NCCR ikiwa aijapata kura ,CUF ikiwa aijapata kura pamoja na TLP

Aidha alibainisha kuwa jumla ya vituo 154 vilikuwa wepo kwa ajili ya kupigia kura na vyote vimekamilisha uchaguzi isipokuwa kimoja ambapo kilifutiwa matokeo hayo na kulazimika kurudiwa ambapo alisema kuwa katika kituo hicho uchaguzi utarudiwa hapo kesho .

mpaka sasa uchaguzi wa uwenyekiti umemalizika ila tumelazimika kurudia uchaguzi katika vituo vitatu ambapo katika vituo hicho kituo kimoja ambacho ni cha Oysterbay uchaguzi utarudiwa kwa watu wote na maanisha uchaguzi wa kuanzia kwa mwenyekiti wa mtaa ,wajumbe  watano pamoja na wajumbe watatu wa viti maalumu huku katika kituo cha AICC -Sekei uchaguzi utarudiwa kwa wajumbe watatu wa viti maalumu ambapo hii inatokana na kura za kufungana kwani wote walipata 31 kwa 31  na katika kituo cha Oldpolisi line ambapo napo uchaguzi utarudiwa kwa watu wawili ambao nao pia  ni wajummbe wa viti waamaalu  walifungana kwa kura 64 kwa 64.

Juma alisema katika uchaguzi wakesho ambao  wanarudia wamejipanga vizuri kusimamia kwani nguvu zote wanazielekeza katika vituo hivyo ambapo alibainisha kuwa katika kila kituo kutakuwa na wasimamizi nane pamoja na ulinzi wa kutosha  .

Aidha alitumia fursa hii kuwashukuru wananchi wate na viongozi kwa kufanya uchaguzi wa amani na kistarabu  pamoja na kuvumiliana huku akiongeza kuwaanamatumaini utulivu huu na uvumilivu walionyesha utaendelea hata katika vituo hivi ambavyo vinarudiwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU