PROFESA TIBAIJUKA ASEMA HAJIUZULU NG'O


1q
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro jijini Dar es salaam leo kuelezea mambo mbalimbali kuhusu Akaunti ya Escrow.
2q
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa wamefurika katika mkutano huo.
3q
Baadhi ya wapiga picha wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwajibika kupata picha katika mkutano huo.
…………………………………………………………………………………………………………
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amesema kamwe awezi kujiuzulu wadhifa wake kwa kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow iliyomkumba kwani tukio alilolifanya ni la mafanikio makubwa kwa upande wa shule zake.Alisema kitendo cha yeye kufanikiwa kuomba na kupokea shilingi zaidi ya bilioni 1.6 kama mchango kwake ni mafanikio makubwa kwa kufanikisha kupata mchango wa kuendesha shule za Sekondari ya Wasichana ya Barbro ya Jijini Dar es Salaam pamoja na Shule ya Wasichana ya Kajumulo ya Mjini Bukoba, hivyo haoni sababu ya kuachia nyadhifa zake.
Profesa Anna Tibaijuka ametoa kauli hiyo mapema leo jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na waandishi wa habari kuendelea kutolea ufafanuzi juu ya sakata hilo lililoitingisha Serikali. Hata hivyo bado anaamini fedha alizopokea ni fedha safi kwani zimetolewa wazi na kwa nia njema na mchangaji wa fedha hizo.
“…Kama Serikali itabainisha kuwa fedha hizo ni haramu basi nitazirejesha Serikalini. Nafanya vitu vingi lakini havionekani na kusisika…naomba tusiwe watu wa kuhukumu bila kumsikiliza anayetuhumiwa 
ni dhambi tena dhambi ya mauti. Binafsi bado nashangaa kwanini Kamati ya Zitto (Mwentekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali) haikuniita kunisikiliza, Kamati ya Zitto kwanini haikuniita kujitetea,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alipoulizwa haoni fedheha kuandamwa na kashfa hiyo na kwanini asijiuzulu kulinda heshima yake na wapigakura wake, alisema haoni fedheha yoyote kwake wala kwa wapiga kura wake. “…Mimi naona ufahari wewe unasema fedheha wewe vipi…labda fedheha itakuja baada ya kubainika aliyetuchangia fedha hizo kaziiba.
Akizungumzia mchango huo wa zaidi ya bilioni 1.6 aliopokea kutoka kwa Mfanyabiashara James Rugemalira wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits ambao ni fedha zinazodaiwa kuchotwa kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow, anasema ni mchango mkubwa ambao hata yeye baada ya kuuona alishtuka na kushukuru sana kwa mtoaji.
“…Kwa kweli ulikuwa mchango mkubwa hata mimi nilishtuka pia na kushukuru sana, baada ya kuuona tulianza kupeana taarifa kuwa kuna neema imetokea. Hata hivyo si sawa kitendo cha baadhi ya watu na vyombo vya habari kuwaaminisha wananchi na taifa kuwa tumeiba fedha hizo, ukiangalia utabaini kuwa hata mimi nimejikuta kwenye mgogoro wa Escrow bila kujua kutokana na kuhangaika kutafuta fedha za wafadhili kwenye shule yetu. 
“…Mimi ni mbunge lakini sikupewa nafasi ya kujitetea kwenye sakata hili, sasa tuache kuwaaminisha wananchi propaganda mbaya tena ya uhaini. Uandishi huu wa kiupotoshaji sio mzuri ni kupotosha jamii. Kimsingi wananchi wanaitaji taarifa za ukweli na si habari za udaku.” alisema Profesa Tibaijuka ambaye amegoma kabisa kujiuzulu.
Anasema kitendo cha wanahabari kuandika kwamba amechota fedha za Escrow ni upotoshaji kwani yeye hakufanya hivyo. Sasa mi nasema wananchi wangu ambao wanateseka kule na kilimo alafu wanasikia nimechota fedha za Escrow wanajisikiaje kwa hili. Kwa hiyo nimekuja hapa kufafanua ili jambo ili lieleweke kwa kweli mimi kama waziri sihusiki katika miamala iliyofanyika. “Wanasema ukweli ukidhihiri uongo utajitenga nimeona kwamba nitoe ufafanuzi. 
*Imeandaliwa na www.thehabari.com

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI