Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ushushaji Mizigo Bandarini - Tanzania International Container Terminal (Ticts), Paul Wallace (kulia) akimkabidhi zawadi kwa timu kapteni wa timu ya Operations ambao waliibuka kidedea dhidi ya Workshop kwa kunyakua makombe yote katika michezo mbali mbali iliyochezwa katika Bonanza la Siku ya Familia iliyofanyika mwishoni mwa wiki ndani ya Kiota cha Kunduchi Wet and Wild jijini Dar es Salaam. Lengo la Siku hiyo ilikuwa ni kuwakutanisha wafanyakazi na familia zao zifurahi kwa pamoja.
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ushushaji Mizigo Bandarini - Tanzania International Container Terminal (Ticts), Paul Wallace akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari.
Meneja Kitengo cha Makontena TICTS, Bw. Donald Talawa akielezea madhumuni ya siku ya familia iliyoandaliwa na TICTS.
Comments