|
Wananchi wa Ludewa wakishusha bati 15o zilizotolewa na mbunge wa Jimbo la Ludewa Deo Fikunjombe kwa ajili y kusaidia kuezeka katika vyumba vinne vya madarasa katika shule ya msingi Ludewa mjini vilivyoezuliwa na kimbunga |
|
Wanafunzi wa shule ya msingi Ludewa mjini wakikusanya bati chakavu |
|
Katibu wa mbunge wa Ludewa Bw Stanley Gowele akipita kando ya vyumba vya madarasa vilivyoezuliwa na kimbunga |
|
Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akisaidia kushusha bati |
|
FIlikunjombe kulia akibeba bati alizozitoa kwa ajili ya shule ya msingi Ludewa mjini |
|
Baadhi ya walimu wa shule ya msingi Ludewa wakimpongeza mbunge Filikunjombe kwa msaada wake |
|
Mbunge wa jimbo a Ludewa Deo FIlikunjombe akifafanua jambo |
|
Wanafunzi wa shule ya Msingi Ludewa mjini wakisomba bati zilizotolewa msaada wa mbunge Filikunjombe |
|
Mbunge Filikunjombe kushoto akishirikiana na wanafunzi wa shule ya Msingi Ludewa mjini kusomba bati |
|
Filikunjombe akishiriki kusomba bati |
|
Mbunge Filikunjombe na viongozi wengine wakisomba bati |
|
WAnanchi wakishiriki kusomba bati |
|
Mbunge Filikunjombe akitazama vyumba vya madarasa vilivyoezuliwa |
|
Filikunjombe akitembelea jengo hilo |
|
Filikunjombe akizungumza na wazazi na walimu wa shule ya msingi Ludewa mjini |
|
Walimu na wazazi wakimpongeza mbunge Filikunjombe kwa msaada wake mkubwa |
|
Filikunjombe akitoa maelekezo kwa kamati ya shule na wazazi |
|
Mkuu wa shule hiyo Bi Agnes Magazi akimwongoza mbunge Filikunjombe kutazama vyumba vya madarasa vilivyoezuliwa |
|
Wananchi wakishirii kusomba saruji iliyotolewa na mbunge Filikunjombe |
|
Diwani wa kata ya Ludewa mjini MOnica Mchilo kushoto na afisa maendeleo ya jamii Ludewa mjini Teopista Kayobo wakishiriki kubeba saruji |
|
Katibu tawala ya Mawengi Bw Dames Kavindi na fisa maendeleo ya jamii Ludewa mjini Teopista Kayobo wakishiriki kubeba saruji |
|
Mbunge Filikunjombe akishuhudia mchanga ukishushwa |
|
Filikunjombe akitoa maelekez o |
|
Filikunjombe akishiriki kuchanganya mchanga na wananchi |
|
Filikunjombe akishiriki kusomba mbao |
Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akishiriki kusoba mbao kwa ajili ya kujenga vyumba vya madarasa vitatu katika shule ya msingi Ludewa mjini vilivyoezuliwa na kimbunga mwanzoni mwa mwaka huu kabla ya kujitolea zaidi ya Tsh milioni 13 kujenga upya vyumba hivyo
|
Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe kushoto na katibu wake Stanley Gowele wakipata chakula cha machana eneo la ujenzi pamoja na wapiga kura wake |
|
Katibu wa mwenezi wa CCM mkoa wa Njombe Bw Honaratus Mgaya kulia na katibu wa mbunge Bw Gowele na mbunge Filikunjombe wakipata chakula
..........................................................................
Na matukiodaimablog
UONGOZI wa serikali ya tarafa ya Mawengi wilaya ya Ludewa mkoani Njombe umempongeza naibu waziri wa maendeleo ya jamii njinsia na watoto Pindi Chana kwa kuchangia kiasi cha Tsh 15000 katika shule ya msingi Ludewa mjini baada ya shule hiyo kupatwa na maafa ya kuezuliwa vyumba vitatu vya madarasa mwanzoni wa mwaka huu.
Afisa tarafa ya Mawengi Bw Damas Kavindi alitoa pongezi hizo leo wakati akipokea msaada wa mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe aliyejitolea kujenga upya vyumba hivyo vya madarasa kwa kwa zaidi ya Tsh milioni 13 .
Katibu tarafa huyo alisemakuwa majengo hayo yaliezuliwa na kimpunga toka februari 28 mwaka huu na kiongozi wa kwanza kufika kutoa pore alikuwa ni Pindi Chana ambae ni mbunge wa viti maalum mkoa wa Njombe na mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa .
" Kweli tunamshukuru sana Pindi Chana kwa kufika mapema zaidi na yeye nyumba yake na shule ni kama mita 200 hivi kwa maana ya kuwa kingozi pekee anayeishi jirani na shule hiyo ......mbali ya kutupa pore kwa maafa hayo aliweza kutuchangia kiasi cha Tsh 15000 kwa ajili ya pore na kutuunga mkono kwa zoezi kubwa lililokuwa mbele yetu"
Pia aliwapongeza wananchi kwa kuchangia kiasi cha Tsh milioni 1.8 kabla ya mbunge wao kujitolea kujenga shule hiyo kisasa zaidi ili kuwaondoea adha ya kuchangishana kwa wananchi wanaozunguka shule hiyo .
Alisema kuwa Kutokana na mahafa hayo wanafunzi 200 kukosa sehemu ya kusomea hivyo kulazimika mikondo miwili kukaa chumba kimoja.
Akishukuru kwa niaba ya walimu wa shule hiyo mkuu wa shule hiyo Bi Agnes magazi alisema msaada huo ni mkubwa na utapelekea wanafunzi hao kupata sehemu ya kusomea.
Alisema kuwa kutokana na vyumba hivyo vitatu kukumbwa na kimbunga pia wanafunzi wa darasa la nne ambalo lipo Jirani na vyumba hivyo vitatu pia walilazimika kuhama vyumba vyao.
Huku kwa Mwenyekiti wa Kamati ya shule Francis Nkwera alisema kuwa Kamati yake baada ya tatizo hilo ililazimika kuzunguka kwa wadau mbali mbali kuomba msaada ili kupata kiasi cha Tsh milioni 13 .1 ili kujenga Nyumba hivyo fedha ambazo hazikuweza kupatikana zaidi ya kupata kiasi cha Tsh milioni 1.8 kwa kipindi chote cha zaidi ya miezi 10 kabla ya mbunge kuingilia Kati .
" msaada wa mbunge wetu ni mkubwa sana kwani pasipo kuingilia Kati kujitolea kujenga vyumba hivi vya madarasa vingemalizika baada ya miaka miwili mbele kutokana na kasi ndogo ya uchangiaji"
Kwa upande wake mbunge Filikunjombe alisema kuwa ameguswa kujitolea baada ya kuona watoto wanapata shida kubwa hivyo kama mbunge asingependa kuona wanafunzi hao wakisoma kwa shida zaidi.
Hivyo alisema kwa upande wake atahakikisha anajenga upya vyumba vyote vilivyokumbwa na maafa hayo na kuwa Ujenzi wake utakuwa wa kisasa zaidi tofauti na majengo mengine shuleni hapo .
Alisema Pindi Ujenzi huo utakapomalizika atahakikisha anaingiza umeme ili kuwawezesha watoto shuleni hapo kusoma kwa raha zaidi.
Hivyo alitaka wazazi kujitolea nguvu zao na suala la mafundi,vifaa vyote vya madukani zikiwemo bati 150 za kutosha kuezeka vyumba hivyo ni jukumu lake . |
Comments