WATANZANIA WASHEREHEKEA MIAKA 53 YA UHURU OAKLAND CALIFORNIA


Balozi wa heshima Mhe. Ahmed Issa (watatu toka kushoto) akibadilishana mawili matatu na mgeni rasmi wa sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara Mhe. Dr. Saidi Mohamed Mtanda (wapili toka kushoto), mbunge wa Afrika Mashariki na mwenyekiti kamati ya kudumu ya huduma za jamii katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Mtanda pia ni Mbunge wa jimbo la Mchinga Mkoani Lindi. Kulia ni Cherry Mke wa Mhe. Ahmed Issa.
Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa akitoa salamu za miaka 53 ya Uhuru na baadae kumkaribisha mgeni rasmi kuhutubia wanaCalifornia katika sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara zilizofanyikia Oakland, California siku ya Jumamosi Desemba 13, 2014.
Mgeni Rasmi Mhe. Dr. Saidi Mohamed Mtanda akihutubia Watanzania Oakland, California siku ya Jumamosi Desemba 13, 2014 katika sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara zilizosherehekewa na Watanzania na amarafiki zao kwenye jimbo hilo la California.
Vikundi mbalimbali vya ngoma za asili vikinogesha sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara California. 
Watanzania na marafiki zao wakifuatilia sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 13, 2014 Oakland, California nchini Marekani.
Watatnzania wa California wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Mhe. Dr. Saidi Mohamed Mtanda.
Kwa picha zaidi bofya

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI