Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (aliyevaa koti la njano) akiwa katika picha ya pamoja na Wastaafu wa Wizara hiyo leo Jijini Dar es Salaam walipokuwa wakiagwa rasmi. Wa pili kulia ni Naibu Waziri, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Juma Nkamia, wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Wizara hiyo, Bi. Sihaba Nkinga na wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara iyo Prof Elisante Ole Gabriel.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akimkabidhi zawadi Bw. Saidi Muhamed Madewa ambaye ni mmoja wa Wastaafu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Idara ya Vijana. Wizara imewaaga wastaafu katika hafla iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam Uwanja wa Taifa. Wa kwanza ni Naibu Waziri, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Juma Nkamia na wa tatu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Sihaba Nkinga.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akimkabidhi zawadi Bi Angella Ngowi ambaye ni mmoja wa Wastaafu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Wizara imewaaga wastaafu katika hafla iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaa Uwanja wa Taifa,wa kwanza kulia ni Naibu Waziri, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Juma Nkamia na wa tatu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Sihaba Nkinga.
Comments