Mwanamuziki wa Nigeria, Innocent Idibia ‘2face’ amejikuta
katika wakati mgumu baada ya picha zinazomuonyesha akifanya mambo ya
chumbani na mwanamke mwengine katika klabu yake ya usiku kuzagaa kama
njugu kwenye mitandao mbalimbali.
Kwa mujibu wa tovuti moja ya udaku nchini humo, imedai
mwanamke anayeoneka katika picha hiyo ni mama wa watoto wa tatu wa 2face
anayeitwa Pero Adeniyi, ambaye amekuwa akipigwa vita mara kwa mara na
mke wa ndoa wa mwanamuziki huyo ‘Annie Idibia’ aliyezaa nae watoto
wawili wa kike.
2face mwenye umri wa miaka 39, ameamua kuzima soo hilo kwa
ku-post picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa na mke wake katika
siku yao ya harusi na kuwataka watu wasipende kuingilia mapenzi yao
kwani watakuja kuujua ukweli na utawaweka huru.
”Our love does not have 2 make sense 2 u. pls go
on with your perfect life and know the true story behind something
before u judge and start making nasty comments based on an orchestrated
story by some blog.U shall know the truth and the truth shall set u free.LYTID uwana idibia”,aliandika 2face
Comments