IPTL yashusha bei ya umeme kwa asilimia 20


KAMPUNI ya ufuaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ikiwa chini ya uongozi wa kampuni ya Pan African Power Solutions (T) Limited (PAP) imetangaza kufikia kwa punguzo la bei ya umeme la asilimia 20 baada ya kufanya marekebisho makubwa ya injini za mtambo huo ya masaa 36,000 ikifanya kazi, zoezi iliyokamilika ndani ya mwanka 2014. IPTL pia imetangaza kuwa bei yao ya umeme ikitarajiwa kushuka zaidi kulingana na kushuka kwa bei ya mafuta mazito. 
Marekebisho hayo yaliyotumia zaidi ya Dola za kimarekani milioni 25 yameiwezesha mitambo ya IPTL kuwa katika nafasi nzuri ya kuzalisha umeme wa uhakika kwa kufikia megawati 100 na kuingiza katika gridi ya Taifa mara to baada ya kukamilika kwa zoezi hilo mnamo Desemba mwaka 2014.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bw. Harbinder Singh Sethi, IPTL sasa imepunguza bei ya umeme wake inaoutoza kwa Shirika la ugavi wa umeme Tanzania (Tanesco) ambao sasa utakuwa chini ya bei ya awali iliyokokotolewa ya senti 23 dola za kimarekani kwa Kilowati; huku ikihakikisha kupatikana kwa umeme wa uhakika.
"Tukiwa tunaukaribisha mwaka 2015, IPTL inajivunia kutangaza kuwa imefanikiwa kufanya marekebisho makubwa ya mashine zake ya masaa 36,000 ya kufanya kazi, zoezi iliyokamilika ndani ya mwaka wa 2014. Nimeiomba timu ya IPTL kupanga mapema jinsi gani wanaweza kuongeza juhudi zaidi kufikia marekebisho ya masaa 48,000, katika awamu inayofuata katika mwaka 2015. Tunatarajia uwepo wa IPTL kuwa bora zaidi kwa kuwa sasa tunajipanga kuongeza rasilimali zaidi.
"Hii ni sehemu ya ahadi ya PAP kuhakikisha kuwa IPTL inaendeshwa vizuri na kwa ufanisi. Wakati sasa umefika kwa TANESCO kuwa na uhakika wa kupata umeme wa uhakika wa megawati 100 katika gridi ya taifa wakati wowote utakapohitajika.
"IPTL chini ya PAP haiangalii tu uzalishaji wa umeme wa kutosha, lakini pia ipo makini kuhakikisha kuwa umeme huo wa kutosha unakuwa nafuu. Kwa maana hiyo, tumeamua kushusha bei zetu za umeme kufikia chini ya bei iliyokokotolewa ya hapo awali ya senti 23 dola za kimarekani kwa uniti, ambayo sasa inaleta jumla ya punguzo la bei la asilimia 20 kwa ile iliyokuwa ikitozwa na IPTL  kabla ya PAP kuchukua uongozi," alisema.
Bw. Sethi aliongeza kuwa TANESCO itarajie punguzo zaidi la bei ya umeme kufikia kiwango cha chini ya Senti 8 Dola za kimarekani kwa kila uniti ya umeme mara baada ya mitambo ya IPTL kupanuliwa na kufikia uzalishaji wa megawati 500 mitambo yake ikitumia gesi asilia.  
Alisema kuwa mpango wa upanuzi wa mitambo hiyo unaendelea vizuri, akiongeza kuwa iko katika hatua za awali za uchanganuzi na upimaji wa udongo.
"Tunatarajia hatua za upanuzi kwenda haraka ili kuhakikisha kuwa IPTL inatoa huduma bora, ya uhakika na nafuu katika taifa hili. Ningependa kutoka shukrani zangu kwa uongozi wa TANESCO na Gridi ya Taifa kwa kukubali umeme unaozalishwa na IPTL,"alisema.
Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali kutoka TANESCO, bei za umeme zinazotozwa na IPTL kwa sasa zimeshuka na kufikia chini ya Senti 19 Dola za kimarekani kwa uniti za umeme kutokana na kushuka kwa bei ya Mafuta mazito wakati wa kipindi cha ukokotoaji wa bei hizo.
Upatikanaji wa umeme wa uhakika kutoka IPTL tayari umeshathibitika wakati wa kipindi cha sikukuu kilichopita ambapo nchi haikukumbana na mgawo wowote ikilinganishwa na miaka iliyopita ambapo ilikuwa ni kawaida kwa umeme kukatika katika wakati wa msimu wa sikukuu ambapo kunakuwa na mahitaji makubwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI