JACKLINE WOLPER AWATOLEA UVIVU WAANDISHI : SITOKI NA MSANII YEYOTE TANZANIA

Mrembo anayeng’ara katika tasnia ya filamu nchini, Jackline Wolper Massawe amewatolea uvivu waandishi wa habari kwa kueneza habari za uongo ambazo zinaharibu mahusiano yake.
Jackline WolperAkitiririka kupitia ukurasa wake wa Instagra, Wolper amesema hatoki kimapenzi na msanii yeyote wa Tanzania wala haja zake za kimwili hazimalizwi na msanii yeyote hapa Bongo.
Amedai kuwa yupo kwenye mahusiano na mwanaume wake na kwamba wanaheshimiana sana na hawezi kuweka mahusiano yake hadharani maana ni mtu na heshima zake.
”Maandishi ya uwongo, yananiharibia sana uhusiano wangu, Plz sitoki na msanii yoyote Tanzania wala nyege zangu hazimalizwi na msanii yoyote  Tanzania, nina mwanaume wangu, namuheshimu, ananiheshimu, nasipo kuweka  mahusiano yangu hadharani wala mitandaoni maana ni mtu na heshima zake”, aliandika Wolper
Aliongeza : ”Nimeumwa na nyoka mara ya kwanza, so hata jana likinigusa ninashtuka, kikubwa sina mapenzi ya matangazowala mitandaoni, sitaki kuandikwa kwa lolote lisilo la ukweli”.
Sakata hilo limekuja kufuatia muigizaji huyo kuandikwa na baadhi ya magazeti ya udaku kuwa yupo kwenye mahusiano ya siri na hitmaker wa Nakula Ujana, Nay Wa Mitego, licha ya wote wawili kukanusha.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.