Mrembo anayeng’ara katika tasnia ya filamu nchini, Jackline
Wolper Massawe amewatolea uvivu waandishi wa habari kwa kueneza habari
za uongo ambazo zinaharibu mahusiano yake.
Akitiririka
kupitia ukurasa wake wa Instagra, Wolper amesema hatoki kimapenzi na
msanii yeyote wa Tanzania wala haja zake za kimwili hazimalizwi na
msanii yeyote hapa Bongo.
Amedai kuwa yupo kwenye mahusiano na mwanaume wake na kwamba
wanaheshimiana sana na hawezi kuweka mahusiano yake hadharani maana ni
mtu na heshima zake.
”Maandishi ya uwongo, yananiharibia sana
uhusiano wangu, Plz sitoki na msanii yoyote Tanzania wala nyege zangu
hazimalizwi na msanii yoyote Tanzania, nina mwanaume wangu,
namuheshimu, ananiheshimu, nasipo kuweka mahusiano yangu hadharani wala
mitandaoni maana ni mtu na heshima zake”, aliandika Wolper
Aliongeza : ”Nimeumwa na nyoka
mara ya kwanza, so hata jana likinigusa ninashtuka, kikubwa sina mapenzi
ya matangazowala mitandaoni, sitaki kuandikwa kwa lolote lisilo la
ukweli”.
Sakata hilo limekuja kufuatia muigizaji huyo kuandikwa na
baadhi ya magazeti ya udaku kuwa yupo kwenye mahusiano ya siri na
hitmaker wa Nakula Ujana, Nay Wa Mitego, licha ya wote wawili kukanusha.
Comments