Hali imeonekana kuwa si shwari katika lebo ya Cash Money, baina ya Rapa Lil Wayne na baba yake wa hiyari ‘Brayan Adams’ A.K.A Birdman hadi kufikia hatua ya kutaka kuburuzana mahakamani.
Upepo mbaya ulianza kuvuma baada ya Lil Wayne kuanza kulalamika juu ya albamu yake mpya ”The Carter 5′‘ kuzidi kucheleweshwa kutoka, ambapo ilitakiwa iingie rasmi sokoni mwishoni mwa mwaka jana.
Kama hiyo haitoshi, Mapema wiki hii, Weezy aliamua kuwaomba
msamaha mashabiki kutokana na kuchelewa kutoka kwa albamu hiyo kupitia
mixtape yake mpya ”Sorry 4 The Wait 2” ambapo ndani yake amem-diss mtu mzima Birdman kwenye ngoma inayoitwa Coco na kujigamba kwamba yeye ni jeshi la mtu mmoja.
“All I got is Young Money, no more Cash
nigga,” “Who kept this s**t together? N***a, me, that’s who! Who was
there when n***as left? N***a, me that’s who!” Cash Money is an army,
I’m a one man army!“.
Hata hivyo Birdman ameendelea kushikilia msimamo wake wa
kutotaka kuiachia albamu ya rapa huyo mpaka siku atakayoamua yeye kuitoa
na kudai kuwa Weezy bado yupo chini ya mkataba na lebo yake.
Hali iliyompelekea Weezy kuanza kutafuta msaada wa kisheria
wa kutaka kuiomba mahakama iweze kumsaidia kutoka katika lebo ya Cash
Money na kutokuwa chini ya utawala wa Birdman ambaye ameendelea
kuishikilia albamu yake.
Akiamini kuwa bado anamdai Birdman kiasi cha dola milioni 8
kama sehemu ya malipo ya awali kwa ajili ya albamu hiyo huku kukiwepo na
tetesi za Rapa huyo kutaka kuhamia katika lebo ya No Limit
inayomilikiwa na Master P.
Endelea kutembelea Blogu yako ya kijanja ya Bamiza.com kwa
muendelezo wa habari hii na nyinginezo kibao zinazowahusu mastaa
mbalimbali wa hapa bongo na nje.
Comments