Mfalme wa Saudi Arabia, Abdullah Bin Abdulaziz amefariki Dunia akiwa hospitalini nchini humo.
Tamko la kifo cha mfalme huyo, limetolewa na kaka wa mfalme huyo aitwae Salman ambaye nae aliwahi kuwa mfalme.
Kabla ya tamko hilo televisheni ya taifa ya Saudi ilikatiza
matangazo yake na kuweka nyimbo za Quaraan kama ishara ya kifo cha
kiongozi wa juu wa ufalme.
Mfalme Abdulrahi amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 90 na
alilazwa hospitalini kwa wiki kadhaa tangu Desemba mwaka jana kutokana
na maambukizi kwenye njia ya hewa.
”His Highness Salman bin Abdulaziz Al Saud and
all members of the family and the nation mourn the Custodian of the Two
Holy Mosques King Abdullah bin Abdulaziz, who passed away at exactly 1
a.m. this morning,” alisema Salman
Viongozi mbalimbali Duniani wanaendelea kutuma rambirambi zao kwa familia ya marehemu anayetarajia kuzikwa baadae hii leo.
Comments