Soko
Kuu la Morogoro likiwa limezingirwa na maji jana baada ya mvua kubwa
kunyesha na kusababisha mafuriko katikati ya mji kutokana na mto Kikundi
kujaa mchanga.Mvua
kubwa zilizonyesha kwa muda mfupi mjini Morogoro zimesababisha mafuriko
baadhi ya barabara kushindwa kupitika na maji kujaa katika baadhi ya
maduka. Wakazi
wa mji wa Morogoro wakizungumzia mafuriko hayo wamelalamikia
miundombinu mibovu ya barabara kutokana na kuziba kwa mitaro ambapo
wameitaka halmasauri ya mji wa Morogoro kuzibua mitaro hiyo huku baadhi
ya wafanyabiashara wakilalamikia kupata hasara
Katika
mto kikundi uliopo mjini Morogoro umepoteza uelekeo na kumwaga maji
katika soko kuu la mji wa Morogoro na kusababisha maji kujaa katika
maduka huku baadhi ya magari yakiingia kwenye mitaro na baadhi ya
bodaboda zikiwa na abiria zime zama katika majina kulazimika kuvutwa.
Kaimu
mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro Phelemon Magesa akizungumzia
alalamiko hayo ya wananchi hao amesema manispaa wanajitahidi kufanya
usafi lakini tatizo liko kwa wananchi wemyewe kutupa taka kwenye mitaro
na kusabisha mitaro hiyo kuziba na maji kupoteza ueleko na kujaa katika
makazi ya wananchi
Comments