WAZIRI DR. FENELLA MUKANGARA AKUTANA NA JUKWAA LA WAHARIRI

      

unnamedWaziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiwaeleza wahariri wa vyombo vya habari nchini wajibu na umuhimu wa vyombo vya habari katika mchakato huu wa upatikani wa katiba mpya ikiwemo kutoa elimu kuhusu umuhimu wa mchakato huu kwa mustakabali wa Taifa pia alivipongeza vyombo vya habari katika elimishaji wa wananchi katika mchakato wa Bunge Maalum la Katiba, Wakati wa Mkutano na Wahariri wa Vyombo vya Habari jana Jijini Dar es Salaam.
unnamed1Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Absalom Kibanda akiongea wakati wa mkutano uliowakutanisha wahariri wa vyombo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamduni na Michezo ambapo Dkt. Fenela Mukangara ambapo waliwataka wahariri kuwa wamoja katika masuala ya kitaifa hasa yatakayopelekea kuibomoa nchi yetu pia aliwaasa wahariri kutumia kalamu zao vizuri kuwaelimisha wananchi katika mchakato huu wa kuelekea upatikaji wa Katiba Mpya kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene, Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mh.Angela Kairuki na Mwisho ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara jana Jijini Dar es Salaam.
unnamed3Mzee Kingunge Ngombale-Mwiru akiongea na wahariri wa vyombo vya habari ambapo ambapo aliwaeleza kuhusu umuhimu wa upatikanaji wa katiba mpya kwa maendeleo ya Taifa ikiwa katiba iliyopendekezwa imezingatia Masuala muhimu ya ukuzaji uchumi wan chi pia uzingatiaji wa makundi mbalimbali katika jamii na alisisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kuelekea upatikanji wa katiba mpya kwani katiba ni chombo cha ukombozi wa nchi.
unnamed4Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Absalom Kibanda akisamiana na Mzee Kingunge Ngombale-Mwiru wakati wa mkutano wa wahariri wa vyombo vya Habari na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara.
unnamed5Mh. Hamadi Rashid Muhamed akiwaeleza wahariri wa vyombo vya habari ambapo alieleza furaha yake kwa katiba inayopendekezwa kujikita katika kutatua changamoto za muungano zitakazopekea kuimarika kwa muungano wa Tanzania bara na Zanzibar.
unnamed6Baadhi wa Wahariri wa Vyombo vya Habari nchini Wakifuatilia Mada zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.