Kilichosababisha kufutwa au kutupwa kwa kesi ya Zitto Kabwe dhidi ya CHADEMA ni technicalities tu. Hii ni baada ya mapingamizi 5 kukubaliwa. Kwa hiyo hata shauri la msingi halikusikilizwa. Kwa mfano.
1. Kesi kufunguliwa mahakama kuu haikuwa jambo sahihi kwani kesi hiyo ilipaswa kufunguliwa mahakama ya wilaya au mahakama ya hakimu mkazi (resident magistrate) kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa kesi za madai.
2. Kesi ilikosewa kufunguliwa mahakama kuu registry kuu (main registry) badala ya mahakama kuu kanda ya Dar-es-Salaam (Dar-es-Salaam Registry).http://www.tanzaniaclassic.com
Comments