KINANA AHUTTUBIA KONGWA NA KUWATAKA VIONGOZI WANAOSABABISHA VIFO VYA WATU WAWAJIBIKE MARA MOJA

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutrano wa hadhara katika Kata ya Mkoka,  wakati wa ziara yake katika Jimbo la Kongwa,mkoani Dodoma leo. Kinana yupo mkoani Dodoma kwa ziara ya siku tisa ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, kuimarisha uhai wa chama na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi. Kinana amewataka viongozi na watumishi wa Serikali wanaosababisha vifo vya watu hata kifo cha mtu mmoja ama mtoto wawajibike mara moja na kushitakiwa.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA WA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mkoka, Jimbo la Kongwa, ambapo aliwataka wananchi kuvipuuza vyama vya siasa akidai havina huruma nao, kwa vile vinawahamasisha kuingia kwenye maandamano yanayozaa vurugu na hatimaye mauaji.
 Msafara wa Kinana ukivuka mto ulipokuwa unaingia katika Kata ya Mkoka wakati za ziara yake katika Jimbo la Kongwa.
 Katibu Mkuu wa CCM akitembea pekupeku alipovua viatu wakati akienda kushiriki kupapalia shamba la Alizeti la la Kijiji cha Iduo Wilayani Kongwa.
 Komredi Kinana akiwa na viongozi wengine wa CCM pamoja na wananchi wakishiriki kupalilia shamaba la alizeti la Kijiji cha Iduo, wakati wa ziara yake katika Jimbo la Kongwa, mkoani Dodoma.
Komredi Kinana akilakiwa na kikundicha ngoma wakati wa mapokezi ya kuingia Jimbo la Kongwa, akitokea  Wilaya ya Mpwapwa, wakati wa ziara yake mkoani Dodoma.
 Msafara wa Komredi Kinana ukipita katika moja ya vijiji wakati wa ziara yake katika Jimbo la Kongwa.
 Komredi Kinana akisaidia kumtwisha ndoo ya maji Subilaga Bukuku baada ya kuzindua mradi wa Maji katika Kijiji cha Malali, wilayani Kongwa leo.
 Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kongwa, Job Ndugai 9kulia0 akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana walipotoka kushiriki ujenzi wa vyumba vya madarasa na hosteli ya Shule ya Msingi wilayani Kongwa.
 Kikundi cha ngoma cha akina mama kikitumbuiza wakati Komredi Kinana alipokwenda kushiriki ujenzi wa zahanati ya Kijiji Njoge, jimboni Kongwa.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia katika Kijiji cha Njoge ambapo alishiriki ujenzi wa Zahanati ya Kijiji hicho.
 Komredi Kinana akishiriki ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Njoge, Jimbo la Kongwa. Zahanati hiyo imejengwa kwa nguvu za wananchi.
 Komredi Kinana (kulia) akijadiliana jambo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye (katikati) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha CCM Mawasiliano ya Umma, Daniel Chongolo.
 Komredi Kinana akiwapungia wananchi alipokuwa akiingia kuhutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mkoaka, Jimbo La Kongwa.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Luteni Chiku Galawa akisalimia wananchi wakati wa mkutano wa hadhara katika Kata ya Mkoka.

 Kikundi cha ngoma za utamaduni cha Kifaru kikitumbuiza wakati wa mkutano, huo.

 Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa akihutubia katika mkutano huo
 Mama mwenye jamii ya kimasai akimkabodhi zawadi ya fimbo Komredi Kinana
 Wananchi wakimsikiliza kwa makini wakati Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mkoka
 Komredi Kinana akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema Wilaya ya Kongwa, na Katibu Mwenezi wa chama hicho wa Kata ya Ngomai,Mwakang'ata Nyanje akitangaza kujiunga na CCM katika mkutano huo. Kushoto ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
Nape Nauye akiwataka wananchi wanaokiunga mkono Chama Cha Mapinduzi kunyoon mikono juu wakati wa mkutano huo. CCM katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Jimbo la Kongwa imeshinda kwa asilimia 99.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.