Kamishna
wa Polisi Elice Mapunda akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa
Kamishna wa Polisi. Katikati ni Msemaji wa Jeshi hilo Mrakibu Mwandamizi
wa Polisi Advera Bulimba. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao
Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.
Kamishna
wa Polisi Diwani Athumani akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa
Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya
Polisi jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akimpongeza Kamishna wa
Polisi Elice Mapunda mara baada ya kula kiapo mbele yake kufuatia
kupandishwa cheo na Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka
Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi
ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.
Kamishna
wa Polisi Diwani Athumani akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa
Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya
Polisi jijini Dar es Salaam.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi).
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi
ya Ulinzi na Usalama mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, amewapandisha vyeo
maafisa watatu (3) wa Jeshi la Polisi kutoka cheo cha Naibu Kamishina wa Polisi
(DCP) kuwa Kamishina wa Polisi (CP) na maafisa wengine 14 kutoka cheo cha
Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) kuwa Naibu Kamishina wa
Polisi (DCP).
Maofisa waliopandishwa vyeo kutoka cheo cha Naibu Kamishina wa Polisi (DCP)
kuwa Kamishina wa Polisi (CP) ni pamoja na Kenneth Kasseke, Elice Mapunda
na Diwani Athumani.
Maofisa wengine waliopandishwa cheo kutoka Kamishina Msaidizi Mwandamizi
wa Polisi (SACP) kuwa Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) ni pamoja na Godluck
Mongi, Ally Lugendo, Salum Msangi, Faustine Shilogile, Maulid Mabakila,
Albert Nyamhanga, Daniel Nyambabe, Salehe Ambika, Robert Boaz na Gabriel
Semiono. Pia wamo kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu Charles Mkumbo,
kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola, kamanda wa Polisi
mkoa wa Arusha Liberatus Sabas na kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala Maria
Nzuki.
Aidha, mhe. Rais amempandisha Juma Yusuf Msige kutoka cheo cha kamishina
msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi
(SACP).
Kufuatia kupandishwa vyeo kwa maafisa hao wa Jeshi la Polisi, Mkuu wa Jeshi la
Polisi nchini IGP Ernest Mangu katika hafla fupi ya kuwaapisha makamishina hao
wapya, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa
kutambua mchango wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia
na mali zao.
Aidha, IGP Mangu amewapongeza maofisa wote waliopandishwa vyeo na
kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa ili kuwa chachu ya
mabadiliko katika kuimarisha usalama wa raia na mali zao. IGP Mangu aliongeza
kuwa, cheo ni dhamana na kuwataka kuwa mfano mzuri katika utekelezaji wa
majukumu yao na usimamizi kwa walio chini yao.
Imetolewa na:
Advera Bulimba -SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Comments