MAKAMISHNA WA POLISI WAPYA WAAPISHWA


Kamishna wa Polisi Elice Mapunda akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi. Katikati ni Msemaji wa Jeshi hilo Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Advera Bulimba. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Polisi Diwani Athumani akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akimpongeza Kamishna wa Polisi Elice Mapunda mara baada ya kula kiapo mbele yake kufuatia kupandishwa cheo na Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Polisi Diwani Athumani akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi).


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, amewapandisha vyeo maafisa watatu (3) wa Jeshi la Polisi kutoka cheo cha Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) kuwa Kamishina wa Polisi (CP) na maafisa wengine 14 kutoka cheo cha Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) kuwa Naibu Kamishina wa Polisi (DCP).

Maofisa waliopandishwa vyeo kutoka cheo cha Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) kuwa Kamishina wa Polisi (CP) ni pamoja na Kenneth Kasseke, Elice Mapunda na Diwani Athumani.

Maofisa wengine waliopandishwa cheo kutoka Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) kuwa Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) ni pamoja na Godluck Mongi, Ally Lugendo, Salum Msangi, Faustine Shilogile, Maulid Mabakila, Albert Nyamhanga, Daniel Nyambabe, Salehe Ambika, Robert Boaz na Gabriel Semiono. Pia wamo kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu Charles Mkumbo, kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola, kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas na kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala Maria Nzuki.

Aidha, mhe. Rais amempandisha Juma Yusuf Msige kutoka cheo cha kamishina msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP).

Kufuatia kupandishwa vyeo kwa maafisa hao wa Jeshi la Polisi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu katika hafla fupi ya kuwaapisha makamishina hao wapya, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua mchango wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao.

Aidha, IGP Mangu amewapongeza maofisa wote waliopandishwa vyeo na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa ili kuwa chachu ya mabadiliko katika kuimarisha usalama wa raia na mali zao. IGP Mangu aliongeza kuwa, cheo ni dhamana na kuwataka kuwa mfano mzuri katika utekelezaji wa majukumu yao na usimamizi kwa walio chini yao.

Imetolewa na:
Advera Bulimba -SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*