Mama wa Katibu wa Mbunge afariki Dunia, wilayani Kibaha mkoani pwani


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
…………………………………………………….
MAMA wa Katibu wa Mbunge wa Viti Maalum Al Shaimar Kweigyir
Semeni Kingaru, anayeitwa Kibibi Haji Pembe, amefariki Dunia leo saa tano
asubuhi akiwa na umri wa miaka 80.
Semeni Kingaru kulia ambaye ni Katibu wa Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir, akiwa na mama yake mzazi Bi Kibibi Haji, ambaye amefariki Dunia leo asubuhi, wilayani Kibaha, mkoani Pwani.
 
Mama huyo amefariki nyumbani kwake kijiji cha
Misugusugu,wilayani Kibaha, mkoani Pwani, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
 
Mtoto wa marehemu huyo Kingaru ambaye ni Katibu wa mbunge Al
Shaimar aliuambia mtandao huu kuwa mama yake atazikwa kesho saa 10 jioni kijijini
hapo kwa ajili ya kumsitiri.
 
Alisema kuwa kwa wanaopenda kushiriki kwenye msiba huo
watalazimika kushuka katika kituo cha kijiji cha Misugusugu ambapo ndipo sehemu
atakapozikwa marehemu mama yake.
 
Msiba huo wakati unatokea, Kingaru alikuwa nchini Uganda
katika majukumu yake na kulazimika kusitisha shughuli hizo kwa ajili ya kuwahi
msiba wa mama yake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI