MKUU MPYA WA WILAYA YA KINONDONI PAUL MAKONDA AANZA KAZI KWA KASI.


 

 
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Eng. Mussa Natty akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa kwanza kushoto) ambapo alisema miradi ya ujenzi wa maabara katika shule za sekondari katika wilaya hiyo itagharimu zaidi ya sh. bilioni 2. na kuwa ujenzi wake unasimamiwa na waataalamu waliobobea katika shughuli hiyo.
FUPA uliomshinda Waziri wa zamani wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka kuhusu migogoro ya ardhi iliyokithiri katika Manispaa ya Kinondoni Mkuu mpya wa wilaya hiyo Paul Makonda ameahidi kuutafuna.
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Mussa Natty alisema miradi hiyo yote ya ujenzi wa maabara katika shule za sekondari katika wilaya hiyo itagharimu zaidi ya sh. bilioni 2. na kuwa ujenzi wake unasimamiwa na waataalamu waliobobea katika shughuli hiyo.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Eng. Mussa Natty akimuonyesha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda jinsi maabara hiyo ilivyojengwa kwa ubora wa hali ya juu.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa kwanza kushoto) akiongea na baadhi ya madiwani wa Wilaya.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Manzese mara baada ya kumkaribisha shuleni kwake,
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiweka saini ya kumbukumbu mara baada ya kuwasiri.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Eng. Mussa Natty akiendelea kuelezea ujenzi wa maabara.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akishuka kutoka kukagua maabara ya ghorofa inayojengwa katika shule ya sekondari Manzese.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Manzese akitoa maelezo machache kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa kwanza kushoto) mara baada ya kuingia katika maabara inayotumiwa kwa sasa.
Mara baada ya kumaliza ziara yake Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa kwanza kushoto) alifanya majumuisho ya ziara, Ambapo ametoa onyo kwa wale wote waliojenga katika maeneo hayo kuanza kuondoka mara moja kabla hawajafikiwa.
"Moto ninaokuja nao katika suala ili hautazimika nitasimamia mimi mwenyewe kwa kushirikiana na polisi ubomoaji wa majengo yote ambayo yamejengwa katika maeneo ya wazi na yale yaliyotengwa kwa ajili ya shule" alisema Makonda.
Makonda alitoa maagizo hayo katika ziara ya siku moja ya kukagua shughuli za maendeleo katika wilaya yake Dar es Salaam jana.
"Mimi simuogopi mtu nasimamia utendaji wangu wa kazi kila mtu anajua msimamo wangu wa kusimamia jambo na katika suala ili hakuna atakaye salimika " alisema Makonda.
Makonda aliagiza migogoro yote ya ardhi ambayo ipo hivi sasa ianze kushughulikiwa na watendaji wanahusika katika manispaa hiyo kuanzia ngazi ya chini na ametenga kila Ijumaa migogoro ambayo inashindikana ipelekwe ofisini kwake ili kuzikutanisha pande zote zinazohusika kwa ajili ya kusuruhisha migogoro hiyo.
Sambamba na agizo hilo Makonga amewataka wote wa manispaa hiyo kusimamia ujenzi wa maabara kikamilifu na kuagiza kuwa Aprili mwaka huu miradi yote iwe imekamilika."Hatutasubiri mpaka mwezi wa sita kama alivyo agiza wazirin mkuu kumaliza miradi yote ndani ya kipindi hicho nawaagiza mkamilishe maabara zote ifikapo mwezi wa nne na wale wote watakaoshindwa wajipime utendaji wao" alisema Makonda.

Mkuu wa Mkoa wa Kinondoni, Paul Makonda akisaini kitabu cha wageni katika shule ya sekondari Turian iliyopo katika wilaya ya Kinondoni wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya Maabara katika sekondari za Wilaya yake. Aliyesimama nyuma yake ni Mkuu wa shule ya sekondari Turiani Mwalimu Betrice Mhando. PICHA ZOTE NA CATHBERT KAJUNA WA KAJUNASON BLOG.
Mkuu wa shule ya sekondari Turiani Mwalimu Betrice Mhando akitoa maelezo machache juu ya shule yake mbele ya Mkuu wa Wilaya aliyeongozana na viongozi mbali mbali wa Wilaya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI