MKUU WA WILAYA KINONDONI PAUL MAKONDA AKUTANA NA WANA UMOJA WA MAFUNDI MAGARI TEGETA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI DHIDI YA MWEKEZAJI

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akiwa na Viongozi wa Umoja wa Mafundi Magari Tegeta wakati akikagua eneo lenye mgogoro wa ardhi kati ya wanaumoja huo pamoja na mwekezaji alipokwenda kuwasikiliza kuhusu mgogoro huo Dar es Salaam jana.
 DC Paul Makonda akiwahutubia wana umoja huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akiwa na viongozi wa umoja huo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Umoja huo Nationi Ndela akitoa historia ya mgogoro huo mbele ya DC Makonda.
 Baadhi ya mafundi magari katika gereji za Tegeta wakimsikiliza DC Makonda wakati akiwahutubia ili kupata muafaka wa mgogoro huo.
 Baadhi ya gereji zilizopo katika eneo hilo la mgogoro.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda (katikati), akijaribu moja ya mashine ya kuchonga vyuma iliyopo katika eneo hilo.
 Baadhi ya mafundi na wamiliki wa gereji mbalimbali katika eneo hilo la mgogoro wakimsikiliza DC Makonda.
 Wanaumoja hao wakiwa kwenye mkutano huo.
Hapa DC Paul Makonda akizungumza na wananchi wa Bunju B Kitunda ambao nao wanamgogoro na mwekezaji katika eneo hilo.
…………………………………………………………………………………..
 
Dotto MwaibaleMKUU wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda ameanza kufanya juhudu za makusudi za kujaribu kumaliza mgogoro wa ardhi kati ya Umoja wa Mafundi Magari Tegeta dhidi ya mmoja wa wawekezaji wilayani humo.Jitihada hizo ameanza kuzichukua ili kujaribu kumaliza mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu na kudumaza shughuli za maendeleo katika eneo hilo la mgogoro lililopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana na mafundi eneo la  Tegeta zilipo gereji mbalimbali zinazo milikiwa na wanaumoja hao alitoa mapendekezo ya kukutana na viongozi wa umoja na mwekezaji ili kufanya mazungumzo ya pamoja kwa ajili ya kutafuta muafaka wa mgogoro huo.
“Eneo hili tayari mahakama imemtambuwa mmiliki wake ambaye ndio mlalamikaji lakini hata hivyo kuna kila sababu ya kukutana na pande zote pamoja na mwekezaji huyo ili tupate ufumbuzi wa mgogoro huu ili uishe ili shughuli za maendeleo ziweze kuendelea” alisema Makonda.
Akizungumzia mgogo huo Naibu Katibu mku wa umoja huo Nationi Ndela alisema ni wa siku nyingi na kuwa kila wanapokwenda wamekuwa hawafanikiwi ambapo walimuomba mkuu huyo wa wilaya kuwasaidia.
Ndela alisema uwekezaji waliouweka katika eneo hilo unafikia zaidi ya sh.bilioni 35 hivyo ni vizuri serikali ikaliangalia jambo hilo kwa ajili ya kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wa ndani.
Alisema kwamba mwekezaji anayedaiwa kumiliki eneo hilo alikuwa na kiwanda cha kutengeneza mabati aina ya asbesto na mara ya mwisho kufanya uzarishaji wa bati hizo ilikuwa kwenye miaka ya 70 tangu wakati huo eneo hilo lilikuwa wazi.
DC Makonda mbali ya kukutana na wamiliki wa gereji hizo pia alikutana na wananchi wa Bunju B Kitunda ambao nao wanamgogoro wa ardhi na mwekezaji ambapo aliwataka viongozi wa eneo hilo kufika ofisini kwake baada ya sikukuu ya pasaka ili kujua chanzo cha mgogoro huo.
Makonda ilikukabiliana na migogoro ya ardhi katika wilaya yake ameanzisha utaratibu wa kukutana na pande zinazovutana kila Ijumaa ili kuitafutia muafaka.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com) 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU