MWENYEKITI UVCCM MKOA WA MBEYA AWAASA VIJANA

 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna ambaye ni mgeni rasmi katika fainali za ligi ya Tarafa ya Tembela akizungumza na wananchi kabla ya kutoa zawadi.
 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna ambaye ni mgeni rasmi katika fainali za ligi ya Tarafa ya Tembela, akisaini katika kitabu cha wageni kwenye ofisi za vijana Kata ya Tembela.
 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna ambaye ni mgeni rasmi katika fainali za ligi ya Tarafa ya Tembela akisalimiana na baadhi ya viongozi.
 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna ambaye ni mgeni rasmi katika fainali za ligi ya Tarafa ya Tembela, akicheza moja ya kikundi cha ngoma za asili
 Baadhi ya timu za mpira kabla ya kuanza mechi.
 Mwenyekiti wa Mashindano Yohana Monga akibadilishana mawazo na mjumbe wa Mrefa.
 Timu zikiendelea na pilikapilika uwanjani
 Mgeni rasmi akiwa meza kuu pamoja na baadhi ya viongozi.
 Baadhi ya Mashabiki.
 Vikundi vya ngoma vikitoa burudani kwa mashabiki.
Mwenyekiti akiteta jambo na Katibu wa Chama cha Wasioona Mkoa wa Mbeya William Simwalki.


 
VIJANA mkoani Mbeya wametakiwa kutumia gharama za aina yoyote ili kulinda umoja, usalama na amani ya Mkoa pamoja na taifa kwa ujumla kwa kuepuka vitendo vinavyoweza kuashiria machafuko.
 
Hayo yalibainishwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) Mkoa wa Mbeya,Amani Kajuna, alipokuwa akizungumza na wananchi pamoja na wachezaji katika fainali ya ligi ya mpira wa miguu ya Tarafa ya Tembela iliyofanyika jana katika kiwanja cha shule ya Msingi Iwalanje wilaya ya Mbeya.
 
Kajuna alisema ikiwa vijana hawatajitoa kuwa wazalendo kwa nchi yao pindi machafuko yatakapotokea watakapokimbilia mipakani mwa nchi walizopakana nazi majina yatabalidilishwa na kuitwa wakimbizi.
 
Alisema ili kuepuka kuitwa wakimbizi ni lazima vijana ambao ni wengi katika taifa wakajitoa kwa gharama yoyote kulinda amani na utulivu uliopo ikiwa ni pamoja na kuwaogopa wanasiasa kuwadanganya na kuwashawishi kuingia kwenye tabia hatarishi.
 
Aidha Kajuna alitumia muda huo kuwasihi vijana kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ikiwa ni pamoja na kuipigia kura katiba inayopendekezwa.
 
Awali katika mchezi huo wa fainali ambao ulizikutanisha timu za Inyala fc na Iwalanje zote kutoka Tarafa ya Tembela ambapo timu ya Inyala ilishinda kwa changamoto ya mikwaju ya penati 6 dhidi ya penati 5 za Iwalanje fc.
 
Timu hizo zililazimika kupigiana mikwaju ya penati baada ya dakika tisini za muda wa kawaida kuisha kwa bila timu kushindwa kuliona lango la mwenzake.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Mashindano hayo, Yohana Monga, alisema ligi ya Tarafa ilianza Januari tatu mwaka huu ikishirikisha timu 17 kutoka katika Kata tano za Tarafa ya Tembela.
 
Alisema ligi hiyo iliokuwa imedhaminiwa na Mwenyekiti wa UVCCM, Aman Kajuna ambaye pamoja na gharama za zawadi kwa washindi alitoa jumla ya shilingi Milioni 1,250,000.
 
Alizitaja zawadi zilizotolewa kwa washindi kuwa ni mshindi wa kwanza ambaye ni timu ya Inyala shilingi 300,000. Mshindi wa pili ambaye ni Iwalanje shilingi 200,000, mshindi wa tatu shilingi 100,000.
 
Aliongeza kuwa zawadi zingine zilienda kwa mfungaji bora, mwamuzi bora, mlinga mlango bora na mchezaji bora ambao kila mmoja alijinyakulia shilingi 50,000 huku Kamati ikipewa shilingi 300,000 pamoja na mchifu wanne ambao kila mmoja alipewa shilingi 20,000/=.
 
Mwisho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI