BIN SLUM (WA PILI KUSHOTO) NA WADAU WENGINE WA COASTAL UNION WAKISHEREKEA USHINDI WA COASTAL UNION, LEO.
Ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam ni faraja kubwa kwa Coastal Union.
KWani
pamoja na kupoza machungu ya kufungwa mabao 8-0 dhidi ya Yanga,
inasherekea kurejea kwa aliyekuwa mdhamini wake nassor Bin Slum ambaye
ameongoza jahazi.
Bin Slum amesema kweli amerejea Coastal Union na kuzika tofauti zilizojitokeza.
“Pamoja na migogoro yote iliyopita, nimekuwa nikisisitiza mimi ni Coastal Union na siwezi kubadilika.
“Nina
faraja pia, nimerudi na ushindi wa mabao hayo mawili na sasa ni
kujitahidi kwa kushirikiana na wenzangu ili Coastal Union isiteremke
daraja,” alisema akionekana ni mwenye furaha.
Mabao ya Coastal Union katika mechi hiyo yalifungwa na Mkenya Rama Salim na Mnigeria, Bright Obinna.
Comments