Dar Leopards kucheza Mombasa katika raga
Timu ya raga ya Dar Leopards inatarajiwa kusafiri kwenda pwani ya Mombasa, Kenya na kucheza na klabu ya Mombasa Jumamosi katika kombe la Mamba (MHC). Dar Leopards ilishinda kombe hilo mwaka jana
Timu hizo zimewahi kupambana mara kadhaa katika miaka ya nyuma. Kwa mujibu wa viongozi wa Dar Leopards, timu hiyo itaondoka Ijumaa kwa usafiri wa basi siku moja kabla ya mechi.
Raga (rugby) ni miongoni mwa michezo isiyo maarufu sana nchini Tanzania na timu ya taifa ya Tanzania (Twigas) imeshiriki mara kadhaa michuano ya Afrika (CAR) na kupambana na nchi kama vile Kenya, Niger.
Dar Leopards ni miongoni mwa timu kubwa nchini Tanzania, mpinzani wake mkubwa ni ni timu ya Arusha Rhinos.
Comments