MTU mmoja amefariki Dunia na 20 kujeruhiwa katika ajali ya basi la Air Jordan iliyotokea wilayani Nzega Barabara ya kwenda Igunga, mkoani Tabora.
Basi hilo lililokuwa limebeba abiria 60 lilikuwa linatokea Mwanza kwenda Dar es Salaam. Akizungumzia ajali hiyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Kaganda, alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi.
Comments