IAAF:Marekani kuandaa riadha mwaka 2021
Marekani itaanda mashindano ya riadha duniani kwa mara ya kwanza mwaka 2021.
Mji wa Eugene katika jimbo la Oregon ulichaguliwa na shirikisho la riadha duniani IAAF.
Shirikisho hilo lilikiuka sheria za utoaji zabuni.
IAAF limesema kuwa uamuzi huo ni mpango uliofanywa baada ya Gavana wa jimbo la Oregon pamoja na kamati ya Olimpiki ya Marekani kutoa usaidizi wa kifedha.
Mji wa Eugene ulishindwa katika harakati zake zaa kuandaa mashindano hayo mwaka 2019 baada ya mashindano hayo kukabidhiwa mji wa Doha nchini Qatar.
Comments