JKJ AUSIFU USHIRIKIANO WA MAENDELEO NA MAREKANI


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425


Description: Coat of Arms
PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Marekani ni mshirika mkubwa wa Maendeleo Tanzania kwa kuunga mkono shughuli  mbalimbali za maendeleo  na kijamii , ambazo  zimeleta mafanikio na mchango mkubwa  katika kukuza na kuendeleza  nchi na maisha  ya wananchi  kwa ujumla.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo jana tarehe 2 April, 2015 jijini Seattle, katika mhadhara uliondaliwa na taasisi ya World Affairs Council na kuhudhuriwa na wafanyabiashara , wafanyakazi wa taasisi mbalimbali  walimu  na wanafunzi wa shule na vyuo kutoka Seattle.
Rais ametoa  mifano ya kazi na michango inayofanywa  na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) ambalo limekuwa mstari wa mbele katika kuchangia katika misaada ya kiuchumi na kijamii,  misaada ya dharura ya kupunguza makali ya Ukimwi (PEPFER), misaada ya Milenia  inayolenga kuondoa umaskini (MCC), Mpango wa Usalama wa Chakula na Kupambana  na Njaa maarufu kama  Feed the Future na Mpango wa Kusambaza umeme kwa watu wengi zaidi barani Afrika maarufu kama Power Africa.
"Mipango na programu zote hizi zina mchango mkubwa kwa Maendeleo ya Tanzania na Watu wake“. Rais amesema na kuonyesha jinsi mahusiano na ushirikiano wa Tanzania na Marekani ulivyo imara na wa manufaa makubwa.
Katika hotuba yake, Rais Kikwete amesema anatumaini kuwa ziara yake jijini Seattle itakuza mahusiano baina ya watu wa nchi hizi mbili na kuyafanya kukua na kuimarika kwa kupitia uwekezaji na shughuli mbalimbali za pamoja katika sekta za binafsi na biashara.

Rais Kikwete yuko jijini Seattle kwa shughuli za kikazi kwa siku moja ambapo pamoja na mambo mengine ametembelea Makao Makuu ya Taasisi ya Bill and Melinda Gates na kufanya mazungumzo na Bw. Bill Gates.Katika mazungumzo yao, Bw. Gates ameahidi kuendeleza juhudi zake na misaada kwa Tanzania katika sekta za Afya na Kilimo.
"Tunatakiwa kuendeleza ushirikiano wetu nawe kwani sauti kama yako  katika masuala ya Afya na Kilimo ni chache, hivyo tunataka kuendelea kushirikiana nawe". Bw. Bill Gates amemwambia Rais Kikwete.
Rais pia amefanya ziara katika Makao Makuu ya Shirika la kutengeneza ndege la Boeing ambapo amepata maelezo na kutembelea kiwandani na kuona utengenezaji wa ndege unaofanywa na shirika hilo.
Rais Kikwete anaendelea na ziara katika jiji la Washington DC.
...............Mwisho...............
Imetolewa na;

Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais  Msaidizi,
Seattle –Marekani.
2 April, 2015


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI