Lewis Hamilton ajifagilia

Lewis Hailton
Bingwa wa dunia wa mbio za magari ya langalanga wa timu ya Mercedes Lewis Hamilton amesema yeye yupo vizuri zaidi kiakili kuliko mchezaji mwenzake wa timu hiyo Nico Rosberg. Hamilton anaamini kuwa kisaikolojia yupo juu ya Rosberg katika mapambano ya mataji ya msimu huu.
Lewis ameyasema hayo baada ya Nico Rosberg raia wa Ujerumani kumtuhumu mchezaji huyo kutumia mbinu za kumdhoofisha yeye ili ashinde. ‘‘Mara zote huwa nasema kwamba yeye ni bora kiakili lakini nafikiri mimi nipo bora zaidi mwaka huu” alisema Hamilton.
Rosberg alidai kuwa Hamilton ambaye ni raia wa Uingereza alipunguza mwendo makusudi wiki iliyopita katika shindano la China Grand Prix na kusababisha yeye kumgonga kutokea nyuma japo mjerumani huyo amesema jambo hilo limeshapita na kufutika.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI