Mama Kanumba akionesha uso wa huzuni baada ya kufika makaburini kwa ajili ya kumkumbuka mtoto wake marehemu, Steven Kanumba.
MAMA
mzazi wa aliyekuwa msanii nguli wa filamu Bongo Marehemu Steven Charles
Kanumba leo mchana aliongoza ibada fupi kama ishara ya kumbukumbu ya
kifo cha mwanaye kilichotokea miaka mitatu iliyopita, shughuli
iliyofanyika katika makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Katika
hafla hiyo fupi, mama Kanumba akiwa pamoja na ndugu, jamaa na marafiki
wa marehemu, waliwasha mishumaa baada ya kufanya usafi wa eneo la kaburi
lake, kumkumbuka nyota huyo aliyefariki Aprili 7 mwaka 2012.
Comments