Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi kuhusu operesheni tokomeza Jaji(Mstaafu)
Balozi Hamisi Amiri Msumi akimkabithi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
Ripoti ya Uchunguzi wa Tume hiyo katika hafla fupi iliyofanyika ikulu
jijini Dar es Salaam leo.Rais Kikwete aliiteua tume hiyo mwaka jana
kuchunguza tuhuma za uvunjifu wa sheria katika utekelezaji wa operesheni
hiyo
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Ijumaa, Aprili 10, 2015 amepokea Ripoti ya Uchunguzi wa Operesheni Tokomeza
katika halfa fupi ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam.
Mara
baada ya kupokea Ripoti hiyo, Rais Kikwete ameishukuru Tume kwa kazi nzuri na
kuongeza kuwa amefurahi kuwa suala zima la Operesheni Tokomeza sasa limefika
mwisho wake.
Aidha,
Rais amesema kuwa Serikali itaisoma
Ripoti hiyo na katika wiki mbili itatoa maelezo ya jinsi Ripoti hiyo
itakavyoshughulikiwa.
Rais
Kikwete amepokea Ripoti hiyo kutoka kwa Balozi Jaji (mstaafu) Hamisi Amiri
Msumi, Mwenyekiti wa Tume ambayo Rais
Kikwete aliiteua Mei Mosi, mwaka jana, 2014, na kuitaka ichunguze tuhuma mbali
mbali za uvunjifu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Hadidu za Rejea za Utekelezaji
wa Operesheni Tokomeza.
Aidha,
Rais Kikwete aliipa Tume hiyo jukumu la kupendekeza hatua stahiki za kisheria
za kuchukua dhidi ya watakaobainika kuhusika na uvunjifu huo. Vile vile, Rais
aliiagiza Tume hiyo ishauri namna bora ya utekelezaji wa Operesheni kama hiyo
hapo baadaye.
Rais
Kikwete pia aliipa Tume hiyo Hadidu za Rejea sita ambazo pia ziliainishwa katika Taarifa ya Serikali Nambari 131 ya
2014. Hadidu za Rejea hizo ni kama zifuatazo:
(a)
Kuchunguza namna Operesheni Tokomeza
ilivyotekelezwa;
(b)
Kuchunguza iwapo maafisa waliotekeleza
Operesheni Tomokeza walizingatia sheria, kanuni, taratibu na hadidu za rejea
walizopewa;
(c)
Kuchunguza iwapo maofisa waliotekeleza
Operesheni Tokomeza walivunja sheria, kanuni, taratibu na hadidu rejea
walizopewa.
(d)
Kuchunguza iwapo kuna watu waliokiuka
sheria yoyote wakati wa utekelezaji wa Operesheni Tokomeza na iwapo hatua
zilizochukuliwa na maofisa wa Operesheni Tokomeza dhidi ya wakosaji hao na mali
zao zilikuwa sahihi;
(e)
Kupendekeza hatua zinazostahili
kuchukuliwa dhidi ya maafisa wa Operesheni Tokomeza waliokiuka sheria, kanuni,
taratibu na hadidu za rejea za Operesheno Tokomeza; na
(f)
Kupendekeza mambo yanayopaswa
kuzingatiwa wakati wa kupanga na kutekeleza Operesheni nyingine kama hii, ili kuepuka
malalamiko mengine yasitokee.
Jaji
Msumi amemweleza Rais Kikwete kuwa katika kutelekeza majukumu yake, Tume
ilitembelea mikoa 20 na wilaya 38 na kupokea malalamiko mbali mbali kutoka kwa
wafuatao:
(a)
Viongozi wa Serikali ikiwa ni pamoja
na mawaziri wanne waliojiuzulu kutokana na sakata hilo;
(b)
Watekelezaji wa Operesheni; na
(c)
Walalamikaji/wahanga wa Operesheni.
Jaji
Msumi amemweleza Rais Kikwete kuwa Ripoti ya Tume ina Juzuu kumi, Juzuu ya
kwanza ikiwa ni Muhtasari wa Taarifa ya Tume, Juzuu ya pili ikiwa ni Taarifa
yenyewe ya Tume, Juzuu ya tatu hadi ya tisa ikiwa ni Mwenendo wa Ushahidi
(Proceedings) na Juzuu ya kumi ikiwa ni vielelezo vilivyotolewa na mashahidi.
Mwisho.
Imetolewa
na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
– Dar es Salaam.
10 Aprili, 2015
Comments