ADEBAYOR 'AIANIKA' FAMILIA YAKE....AMUUMBUA HADI MAMA YAKE MPENDA FEDHA KULIKO UTU, ASEMA...

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Arsenal, Emmanuel Adebayor amefunguka kwenye akaunti yake ya Facebook, akielezea kila kitu ambacho amefanya kwa ajili ya ndugu zake na mama yake.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye amekanusha taarifa za kumfukuza mama yake knyumbani kwake Novemba, aliorodhesha kila kitu alichowanunulia familia yake na ndugu zake wakati wa soka lake la kilipwa.
Adebayor amesisitiza kwamba ameamua kuujulisha uma juu ya malumbano na familia yake ili kuzisaidia familia zingine za Afrika kujifunza kutoka kwenye familia yake.
Emmanuel Adebayor uploaded this picture on to his Facebook as well as a lengthy 877-word statement
Emmanuel Adebayor ameweka picha hii Facebook sambamba na taarifa ya maneno 877
Tottenham striker Adebayor denied claims he kicked his mum out of his house back in November 
Mshambuliaji wa Tottenham, Adebayor amekanusha kumfukzua mama yake Novemba mwaka jana 

Mchezaji huyo wa Togo, ambaye alirudishwa katika katika kikosi cha kwanza cha Tottenham dhidi ya Manchester City, Jumapili iliyopita baada ya kukaa benchi kwa miezi miwili, alitumia maneno 877 kuelezea jambo hilo.
Alieleza jinsi alivyolipa kwa ajili ya mama yake kwenda kufanyiwa vipimo London, pia kumuacha dada yake kukaa kwenye nyumba ya dola milioni 1.2 iliyopo nchini Ghana na kumsaidia mmoja wa kaka zake kuanzisha biashara, pamoja na kuwalipia watoto wa kaka yake huyo ada ya shule.
Premier League ace Adebayor (right) recently returned to action after a lengthy spell on the sidelines
Nyota wa Ligi Kuu England, Adebayor (kulia) hivi karibuni amerejea uwanjani baada ya kuwa nje kwa muda mrefu

JUJU NI NINI HASWA?

Juju ni neno linalotumika Afrika Magharini kuutambulisha uchawi. Inasemekana Juju ilianza enzi za utumwa (na ukoloni), lakini bado imeendelea kuwa utamaduni wa Waafrika 
Adebayor, ambaye alihamia England mwaka 2006 baada ya kusajiliwa na mahasimu wa Tottenham, Arsenal, alisema pia alimpeleka mama yake kwa mchungaji wa Nigeria, T. B. Joshua akae wiki kadhaa, lakini aliondoka baada ya siku mbili.
Pia mshambuliaji huyo wa Ligi Kuu England alikosolewa kuhusu marehemu kaka yake Peter, lakini alifunguka kwamba hakuruhusiwa kumuona kaka yake alipokuwa anaumwa na kuambiwa atoe fedha kwa ajili yake.
Mchezaji ambaye alikutana na mshambuliaji wa Chelsea, Didier Drogba kujadiliana matatizo yake, aliongeza kwamba alianzisha mfuko wa hisani Afrika kabla hajafa.
Katika maelezo mbalimbali aliyoweka kwenye mtandao wa Facebook, Adebayor alisema: “Watu wengi wamenishauri kufuata ushauri kwa kutoka kwa Drogba.
“Nilikaa chini na Drogba na ushauri mkubwa aliyonipa ni kufanya kile ambacho kitaniridhisha na kuwa na furaha. Pia niwashauri ndugu zangu Kola Adebayor, Roten De Lux Adebayor na dada yangu Lucia Adebayor wakatafute kazi za kufanya.'
Alifikiria kwamba anahitaji kwenda redio ya Peace FM, Novemba mwaka jana kukanusha maneno ya dada yake Maggie kwamba alimfukuza mama yake kwenye nyumba.
Dada yake Margaret katika mahojiano marefu na redio hiyo ya Peace FM, alidai kwamba sababu ya mchezjai kumfukuza mama take kwenye nyumba hiyo ni kwa kuwa alidhania ni mchawi, lakini mwenye Adebayor, alisema: “Sijamfukuza mama. Aliamua kuondoka mwenyewe.
“Nitakuwaje karibu na mama yangu kama yeye anawaambia watu kwamba mambo yangu hayatakuwa mazuri, hivyo nitaendelea kufanya mambo yangu.”
“Wanatakiwa waache kuchonga, wanatakiwa waache kunifanyia uchawi, waniache mwenyewe. Nilinunua nyumba ya dola milioni 1.2 (shilingi bilioni 2.3) iliyopo eneo ya East Legon kwa huyo anaechonga na kujiita dada yangu. Unaweza kuamini huyo dada ameenda kupangisha nyumba hiyo bila ya kunijulisha?'
Haijakuwa wazi kwamba nani alikuwa anamwambia aache kumfanyia ushirikina mchezaji huyo.

Adebayor recently spoke to Chelsea striker Didier Drogba to seek advice regarding his personal problems 

Adebayor hivi karibuni alizungumza na mshambuliaji wa Chelsea, Didier Drogba juu ya matatizo yake binafsi

Maisha yake; Adebayor, ambaye jina lake kamili ni Sheyi Emmanuel Adebayor, alizaliwa mjini Lome nchini Togo, Februari 26 mwaka 1984.
Mchezaji huyo ambaye wazazi wake ni watu wa jamii ya Yoruba, alikuwa akiichezea klabu yake ya kwanza ya Sporting Club de Lome na kuonekana na wakala wa Metz, ambaye alimchukua kwenda nae Ufaransa mwaka 1999.
Nyota huyo wa Tottenham Hotspur na Togo, amezichezea klabu za Metz, Monaco, Arsenal, Real Madrid na Manchester City.
Adebayor, ambaye ni mkristo ameoa na ana mtoto mmoja wa kike aitwaye Kendra, aliyezaliwa Juni mwaka 2010.
Akizungumzia kuhusiana na imani yake, Adebayor, alisema: “Kila ninachofanya katika maisha yangu nayawekaa kwenye mikono ya Mungu, muumbaji wangu. Amenipa nafasi ya kuwepo pale nilipo mimi na ndiye anaeweza kuchukua kile nilichonacho. Hakuna kitu muhimu kwangu zaidi ya Mungu." Adebayor hakuweza kutembea kwa miaka minne katika maisha yake. Mama yake alimzungusha Adebayor kila sehemu kutafuta tiba.
Mwenyewe alizungumzia mkasa huo na kusema: “Nilikuwa kanisani nikiwa nimelala chini, ilikuwa Jumapili saa 3:00 au 4:00 asubuhi, nilikuwa nikisikia watoto wakicheza nje. Ghafla kuna mmoja akaupiga mpira ndani ya kanisa. Mtu wa kwanza kusimama na kukimbia nilikuwa ni mimi, kwasababu nilikuwa nataka kuupata ule mpira.” Kuanzia hapo mchezaji huyo alinza kutembea baada ya kushindwa kufanya hivyo kwa miaka minne.

TAARIFA YA MAMENO 877 A EMMANUEL FACEBOOK 

Maelezo yake yalisomeka: Tazama, nimezinyamazia hizo habari kwa muda mrefu, lakini leo ni vizuri kushirikiana mambo hayo na nyinyi. Ni kweli mambo ya kifamilia yanapaswa kumalizwa kindugu sio hadharani, lakini nafanya hivi ili familia zingine zipate kujifunza kwa kile ambacho kimetokea kwangu. Pia weka akili mwako kwamba mambo haya hayahusiani na suala la fedha.
Nikiwa na umri wa miaka 17, mshahara wangu wa kwanza kama mchezaji, niliinunulia familia yangu nyumba na kuhakikisha wako salama. Najua nyote mnafahamu kwamba nilibeba tuzo ya ya mchezaji bora wa Afrika mwaka 2008. Nilipanda stejini na mama yangu kumshukuru kwa kila kitu. Mwaka huo huo nilimchukua hadi London kwa ajili ya kuangalia afya yake.
Wakati binti yangu alipozaliwa, tuliwasiliana na mama kumjulisha lakini ghafla alikata simu hakutaka kujua wala kusikia. Nimesoma maelezo yenu, kuna watu wanasema familia yangu inatakiwa tukazungumze na T.B Joshua.
Mwaka 2013, Nilimpa mama yangu fedha ili kukutana na mchungani huyo nchini Nigeria. Alitakiwa kukaa kwa wiki moja; lakini alikaa siku mbili, nilipokea simu kuambiwa kwamba ameondoka.
Ukiachana na hilo, pia nilimpa mama yangu kiasi kikubwa cha fedha kuanzisha biashara ya kupika na vitu mbalimbali. Pia nikawaruhusu kuweka jina langu na picha kwenye mgahawa wao ili waweze kuuza zaidi. Ni kitu gani kingine kijana anaweza akafanya kuiunga mkono familia yake?
Miaka kadhaa iliyopita nilinunua nyumba eneo la East Lagon (Ghana) yenye thamani ya dola milioni 1.2 (shilingi bilioni 2.3). Niliona ni jambo zuri kumruhusu dada yangu mkubwa, Yabo Adebayor kukaa kwenye nyumba hiyo. Pia nilimruhusu mdogo wangu wa kambo (Daniel) kukaa kwenye nyumba hiyo. Miezi michache baadaye, nilikuwa kwenye mapumziko nikaamua kwenda kwenye nyumba hiyo. Nilishangazwa, kuona magari mengi kwenye gereji ya nyumba hiyo. Kumbe dada yangu aliamua kuipangisha nyumba hiyo bila ya mimi kujua. Pia alimfukuza Daniel kwenye nyumba hiyo.
Fikiria kwamba nyumba hiyo ilikuwa na jumla ya vyumba 15. Nilipompigia na kutaka maelezo, alitumia dakika 30 kunisemea maneno mabovu na kunitukana kwenye simu. Nikampigia mama yangu kumuelezea hali hiyo naye alifanya kama dada. Dada huyu ndiye aliesema sina shukrani. Muulize kuhusu gari analoendesha au kile anachouza leo?
Kaka yangu Kola Adebayor, amekuwa Ujerumani kwa miaka 25. Anasafiri kurudi nyumbani mara nne kwa mwaka kwa gharama yangu. Natumia fedha zangu kulipia watoto wake gharama za shule.
Nilipokuwa Monaco, alinifuata na kuniomba fedha aanzishe biashara. Mungu ndiye anaejua kiasi cha fedha nilichompa. Hiyo biashara iko wapi leo?
Wakati kaka yangu Peter alipofariki, nilimtumia Kola kiasi kikubwa cha fedha ili aweze kusafiri kurejea nyumbani. Lakini hakuonekana kwenye mazishi. Laki leo hii kaka huyo huyo (Kola) anawaambia watu kwamba nahusika kwenye kifo cha kaka Peter. Kivipi? Ndio kaka huyo huyo aliyekwenda kuuambia mtandao wa Sun habari ya uongo ili apewe fedha. Pia walituma barua kwenye klabu yangu, nilipokuwa Real Madrid ili niweze kufukuzwa kazi.
Nilipokuwa Monaco nilifikiri kwamba itakuwa vizuri kuwa na familia ya wacheza soka. Hivyo nilihakikisha mdogo wangu Rotimi anajiunga kwenye ‘academy’ ya soka nchini Ufaransa. Katika miezi michache aliiba simu za watu 21 kati ya watu 27 ambao wako kwenye ‘academy’ hiyo.
Sikupaswa kusema lolote kuhusiana na marehemu kaka yangu Peter Adebayor kwasababu hayupo kwa sasa. Mungu ailaze roho yake mahali pema.
Dada yangu Lucia Adebayor aliwaambia watu kwamba baba yangu aliniambia nimpeleke Ulaya. Nampelekaje huyo dada Ulaya wakati kila mmoja yuko hapa.
Nilikuwa Ghana nilipokea taarifa za kuzidiwa kwa kaka Peter. Niliendesha gari kwa kasi sana kwenda Togo ili kuweza kumuona na kumsaidia. Nilipowasili, mama yangu aliniamboa sitaweza kumuoana ila nimpe fedha na atamaliza matatizo yote. Mungu pekee ndio anajua nilimpa kiasi gani cha fedha siku ile. Watu wanasema sikufanya chochote kumsadia kaka yangu Peter. Mimi ni mpumbavu kuendesha gari saa kwenye Togo bila ya sababu?
Niliitisha mkutano mwaka 2005 ili kusaidia matatizo ya familia yangu. Nilipouliza kuhusu maoni yao, walisema niwajengee kila mtu nyumba yake na kila mmoja nimpe mshahara kila mwezi. Leo bado niko hai lakini tayari wamekwishamaliza kila kitu changu, hivi nikifa itakuwaje.
Kwasababu zote hizo ilinichukua muda kuanzisha mfuko wa hisani barani Afrika. Kila mara najaribu kusaidia watu wenye mahitaji, lakini wao wote wanaona ni jambo baya.
Naandika haya sio kuwaaibisha ndugu zangu, bali nataka familia zingine za kiafrika zipate kujifunza kutoka katika matatizo hayo ambayo mimi nayatpita. Asanteni.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.