[caption id="attachment_57718" align="aligncenter" width="800"] Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem wa (kwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuzungumzia Maadhimisho ya Siku ya kupinga ugonjwa wa Fistula Duniani. Wa pili kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Tanzania, Brenda Msangi.[/caption]
[caption id="attachment_57722" align="aligncenter" width="800"] Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Tanzania, Brenda Msangi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuzungumzia Maadhimisho ya Siku ya kupinga ugonjwa wa Fistula Duniani. Wa kwanza kulia ni Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem.[/caption]
[caption id="attachment_57723" align="aligncenter" width="800"] Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem wa (kwanza kulia) akiwapongeza baadhi ya akinamama waliougua fistula na kupona na kuwezeshwa kibiashara na sasa wanafanya ujasiliamali.[/caption]
[caption id="attachment_57719" align="aligncenter" width="800"] Baadhi ya waandishi wa habari wakijitahidi kupata habari katika ukutano huo.[/caption]
[caption id="attachment_57720" align="aligncenter" width="800"] Mmoja wa waathiriwa wa ugonjwa wa Fistula, Lidya Makanda aliyepata matibabu na kupona akionesha kipeperushi kilichookoa maisha yake baada ya kukisoma na kwenda hospitali kutibiwa ugonjwa huo.[/caption]
[caption id="attachment_57721" align="aligncenter" width="800"] Baadhi ya madaktari wanaotoa matibabu ya ugonjwa wa Fistula katika Hospitali ya CCBRT Tanzania wakiwa katika mkutano huo na wanahabari.[/caption]
[caption id="attachment_57724" align="aligncenter" width="800"] Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem na Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Tanzania, Brenda Msangi wakipiga picha ya pamoja na akinamama waliougua fistula na kupona na kuwezeshwa kibiashara na sasa wanafanya ujasiliamali.[/caption]
[caption id="attachment_57725" align="aligncenter" width="726"] Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem (kulia) akihojiwa na moja ya wanahabari mara baada ya mkutano huo.[/caption]
[caption id="attachment_57726" align="aligncenter" width="800"] Mwandishi wa habari wa kituo cha ITV, Sam Mahela (mwenye kipaza sauti cha ITV) akipiga picha na akinamama waliougua fistula na kupona na kuwezeshwa kibiashara na sasa wanafanya ujasiliamali.[/caption]
[caption id="attachment_57727" align="aligncenter" width="600"] Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem na Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Tanzania, Brenda Msangi wakipiga picha ya pamoja mara baada ya mkutano na wanahabari katika Hospitali ya CCBRT Jijini Dar es Salaam Tanzania.[/caption]
Na Joachim Mushi, Dar es Salaam
ZAIDI ya akinamama 3,000 nchini Tanzania huugua ugonjwa wa fistula mara baada ya kujifungua kila mwaka, huku sababu kubwa ya kupatwa na ugonjwa huo ikiwa ni huduma duni za afya ya uzazi hasa zile huduma za dharura kwa wajawazito wanapokuwa wakijifungua.
Taarifa hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dk. Natalia Kanem alipokuwa akizungumza na wanahabari juu ya maadhimisho ya Siku ya kupinga ugonjwa wa Fistula Duniani.
Lakini robotatu ya wagonjwa hao hawana uelewa wa kwamba wanaweza kupata matibabu na kupona kabisa ugonjwa huo. Ipo haja ya kuongeza bajeti ya huduma kwa wahusika na kutoa elimu zaidi ili kusaidia jamii hii inayoangamia kila kukicha kwa matatizo ya fistula. Wakinamama na wasichana ambao hukumbwa na matatizo ya fistula wamekuwa wakipata changamoto kubwa baada ya kutengwa na familia zao na wengine kuvunjika ndoa zao kutokana na hali ya kuvuja mkojo muda wote huku wakitoka na harufu kali. Alisema ili kuunga mkono juhudi za kukabiliana na ugonjwa wa fistula.
Hata hivyo ili kupambana na ugonjwa huo, Dk. Kanen alisema kuanzia mwaka 2003 UNFPA na wadau wenzake ilizinduwa kampeni ya dunia nzima kuhakikisha inazuia ugonjwa wa fistula (Grobal Campaign to End Fistula) mradi ambao kwa sasa unafanya kazi kwa zaidi ya mataifa 50 ulimwenguni huku ukijikita kwa kuzuia, kutibu na kuwasaidia kiuchumi waathirika wa ugonjwa huo.
Hali hiyo imewafanya washindwe kujiendeleza katika shughuli zao za kila siku za kujiongezea kipato, Takribani akinamama 800 wanakufa kila siku dunia nzima kutokana na matatizo ya uzazi huku 20m kati yao wakijikuta wameathiriwa vibaya na ugonjwa hatari wa fistula. Inakadiliwa kuwa kati ya akinamama 50,000 hadi 100,000 wanaosumbuliwa na ugonjwa wa fistula ni 20,000 tu ndio hufanikiwa kupata matibabu ya ugonjwa huo kwa mwaka.
Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Tanzania, Brenda Msangi akizungumza na wanahabari kuzungumzia maadhimisho hayo yanayoanza tarehe 23 Mwezi Mai, 2015 alisema hospitali hiyo na washirika wake inasapoti maeneo manne ya wagonjwa wa fistula ambayo awali yalionekana ni changamoto kwao.
Aliyataja maeneo hayo ni pamoja na Matibabu kwa wagonjwa, Gharama za Usafiri, Gharama za Chakula na Gharama za Malazi ili kumsaidia mgonjwa kuweza kukabiliana na changamoto hizo. "...Tunaomba kila mmoja kuanzia ngazi za familia watoe elimu kwa wahusika waje hospitalini kupata matibabu mapema kwani ugonjwa huu unatibika," alisema Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT, Brenda Msangi.
MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA
1. Wahiraki, Hawa ni wanawake wa jamii ya Wahiraki wa napatikana kaskazini mwa Tanzania wamezagaa mikoa ya manyara ni weupe Wana Umbo zuri wanavutia kwa Macho. 2. Warangi, Hawa ni wanawake jamii ya Warangi ni wazuri nywele zao ni asili ya waraabu weupe sura nzuri wanapatikana kondoa. 3. Wanyiramba. Hawa ni warembo Sana sura matata wanapatikana mkoa wa singida kaskazini, usipokua makini utawafananisha na wanyaturu 4. Wamasai, kabila hili wanawake wazuri sio wengi Sana lakini ukikutana na sampuli Tatu au nne hivi utauza hata boxa kuongezea mahari wamezagaa Sana Arusha 5. Wahaya, hawa nao ni jamii ya Kanda ya ziwa maumbile Yao Kuna weupe miguu Yao ya bia shape matata wamejaa Sana bukoba. 6. Wanyaturu, Hawa wanafanana na Wanyiramba wanapatikana singida hasa ikungi na manyoni weupe wanavutia 7. Wapare, Hii ni jamii ya kabila la Wapare wanapatikana moshi wilaya ya same wako vizuri usicheze kabisa na hili kabila shape nzuri. 8 .Wamakonde, Hawa wanapatikana kusini mwa Tanzania ni kab
Comments