Hatimaye mgomo wa madereva wa mabasi ulioingia siku ya pili, umemalizika baada leo mchana madareva kukubali kurudi kuendesha tayari kwa safari za kwenda mikoani kutoka Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo, Dar es Salaam kuanzia saa 7 mchana.
Madereva hao inadaiwa wamekubali baada ya serikali kusikiliza kilio chao na kuahidi kukifanyia ufumbuzi wa haraka. Pia Waziri Mkuu ameunda Tume ya Watu 13 ya kushughulikia matatizo ya madereva wa mabasi, Daladala na malori nchini.
Pia mazungumzo ya madereva na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paulo Makonda na Waziri Mkuu Kivuli, Freeman Mbowe walikwenda na kufanya nao mazungumza yaliyochangia kuwashawishi madareva hao kuanza tena safari.
Habari zilizotufikia punde kutoka mikoani ni kwamba tayari nako mgomo umeisha na mabasi yameanza safari kwenda mikoa mbalimbali.
Madereva hao inadaiwa wamekubali baada ya serikali kusikiliza kilio chao na kuahidi kukifanyia ufumbuzi wa haraka. Pia Waziri Mkuu ameunda Tume ya Watu 13 ya kushughulikia matatizo ya madereva wa mabasi, Daladala na malori nchini.
Pia mazungumzo ya madereva na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paulo Makonda na Waziri Mkuu Kivuli, Freeman Mbowe walikwenda na kufanya nao mazungumza yaliyochangia kuwashawishi madareva hao kuanza tena safari.
Habari zilizotufikia punde kutoka mikoani ni kwamba tayari nako mgomo umeisha na mabasi yameanza safari kwenda mikoa mbalimbali.
Comments