Mhifadhi utalii katka hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA),Eva Mallya akizungumza juu ya ofa iliyotangazwa na hifadhi hiyo ya kupanda mlima huo kwa siku moja na kurudi hadi kilele cha Shira.
Afisa
masoko wa KINAPA ,Antypas Mgungusi akisistiza jambo wakati akizungumzia
juu ya ofa ya safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro huku akishauri wenye
sherehe zao kutumia nafasi hiyo kupanda Mlima huo kwa ajili ya kufanya
sherehe zao,alitaja sherehe ambazo zinaweza fanyika katika hifadhi hiyo
ni pamoja na wale wenye kukumbuka siku zao za kuzaliwa wanaweza fanya
hivyo wakiwa kileleni,lakini pia kwa wale wanaoenda Honey Moon baada ya
ndoa pia wameshauriwa kufanya hivyo katika kipindi hiki cha ofa.
Baadhi ya watalii wa ndani wakielekea katika kilele cha Shira safari ambayo inatajwa asilimia 70 wanaenda kwa usafiri wa gari.(P.T)
Ukiwa katika hifadhi hiyo utafurahia mandhari mbalimbali za mlima huo.
Wengine wanaweza pia kupanda na watoto wao.
Hivi ndivyo safari ya mwisho huwa.
Njiani utakutana na uoto mbalimbali wa asili .
Zipo tenti kwa ajili ya watalii wanaoendelea na safari.
Waliofanikiwa kufika kilele cha Shira hawakusita kuonesha furaha zao kwa kucheza .
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
IDADI ya
watalii wanaotembelea hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA)
imeongezeka kutoka 37,000 hadi kufikia 51,287 ndani ya kipindi cha miaka
10 huku asilimia 4 na sita kati yao wakiwa ni wazawa.
Asilimia
hiyo inatajwa ni ya watanzania ambao wamekuwa wakipanda Mlima huo kwa
muda wa siku moja hali inayoilazimu uongozi wa hifadhi hiyo kuendelea
kuhamsisha wananchi kutembelea hifadhi zetu ili kujionea urithi
tuliopewa na Mungu.
Mhifadhi
utalii wa KINAPA,Eva Mallya alisema katika kuhamasiosha utalii wa ndani
,KINAPA imeandaa zoezi maalumu ambalo litadumu kwa muda wa siku nne kwa
watanzania walio walio karibu na mlima kuweza kuupanda kwa muda wa siku moja na kurudi.
“Tumeandaa
zoezi rahisi kwa kila mmoja mwenye nafasi aweze kupanda,sehemu kubwa
itakuwa ni kwa kutumia gari ambapo walio tayari watachukuliwa na gari
hadi eneo fulani kabla ya kutembea umbali mdogo na kutizama uwanda wa
Shira katika mlima Kilimanjaro.”alisema Mallya.
Alisema
zoezi la uandikishaji kwa ajili ya watakao penda kupanda katika mlima
huo tayari limeanza katika vituo vilivyoko jirani na Duka la Maua
mkabala na Rafiki Supermarket ,Hosptali ya rufaa ya KCMC na njia Panda
ya Himo.
Mallya
alisema mpandaji atapaswa kujitegemea kwa Sweta na Jacket kwa ajili ya
baridi ,suruali raba pamoja na chakula huku mhusika akitakiwa kulipia
kiasi cha sh 15,000 kama kiingilio cha hifadhini.
Kwa
upande wake afisa masoko wa KINAPA,Antypas Mgungusi alisema safari ya
kupanda mlima Kilimanjaro imekuwa ikitumiwa na baadi ya watalii kufanya
matukio ya kihistoria ikiwemo kufunga ndoa na wengine kuadhimisha siku zao za kuzaliwa wakiwa kileleni.
“Imezoeleka
kuwa watu wanapokuwa na matukio yao yakiwemo ya mikutano,au Honey moon
baada ya ndoa na siku za kuzaliwa wamekuwa wakifanya sherehe zao
mijini,lakini kuna maeneo mengine kama haya ya hifadhi kufanyia mambo hayo”alisema Mgungusi.
Hifadhi
ya taifa ya Mlima Kilimanjaro ni maarufu duniani kwa kuhifadhi barafu
kwa kipindi cha mwaka mzima licha ya kupitiwa na mstari wa Ikweta huku
ukiwa ndio mlima pekee uliosimama peke yake ukilinganisha na milima mingine duniani.
Mwisho.
Comments