IVO MAPUNDA ATIMKIA OMAN, MIPANGO YA MUSLEY HIYO

MAKIPA wote wa Simba SC, wakiongozwa na ‘mkubwa wao’ Ivo Mapunda watakwenda mafunzoni nchini Oman.

Ivo pamoja na kipa wa pili, Hussein Sharrif ‘Casillas’ na makipa wa timu ya vijana wanaokomazwa kikosi cha kwanza, Peter Manyika na Dennis Richard wanatarajiwa kuondoka wakati wowote kwenda Oman.
BIN ZUBEIRY inafahamu kwamba mipango ya makipa hao kwenda mafunzoni, imefanywa na mmoja wa wafadhili wa timu hiyo, Musley Al Ruweh.
Ivo Mapunda anatarajiwa kuwaongoza makipa wenzake wote Simba kwenda Oman kwa mafunzo maalum

Musley ambaye pia amegharamia safari ya kwenda Oman kwa kocha wa makipa Meja na kocha Msaidizi, Suleiman Matola hakupatikana alipotafutwa kuzungumzia safari hiyo, lakini BIN ZUBEIRY inafahamu ni wakati wowote kuanzia sasa.
Makipa hao wanatarajiwa kwenda kunufaika na mafunzo ya kocha wa makipa aliyebobea, Haroon Amur Al Siyabi ambaye mara kadhaa huja nchini kuwanoa makipa wa Simba SC.
Matola yeye ambaye kwa sasa anaendelea na mafunzo ya ukocha Dar es Salaam, anatarajiwa kwenda kupatiwa programu maalum ya kujiendeleza zaidi kielimu nchini humo.
Musley kulia ndiye amefanikisha safari ya makipa wa Simba SC mafunzoni Oman

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA