JESHI LA POLISI MKAONI IRINGA LINAWASHIKILIA WANANCHUO 89 WA CHUO KIKUU CHA IRINGA

Wanafunzi  wa  Chuo  Kikuu cha Iringa  wakiwa katika mgomo  leo kutokana na kutopata mkopo kwa wakati ambapo inapelekea kushindwa  kabisa  kuendesha maisha  yao  chuoni  hapo baada ya  serikali  kupitia  bodi ya  mikopo  kuwacheleweshea  pesa  zao.
Viongozi  wa  serikali ya wanafunzi wa Chuo  Kikuu cha Iringa  wakiwatuliza  wenzao  leo baada ya mgomo wa wanachuo wa chuo cha RUCU kugoma wakishinikiza kupewa mikopo yao ili kuendesha maisha chuoni hapo.
Mkuu  wa chuo  kikuu ya Iringa Prof Joshua Madumulla akizungumza na wanafunzi hao baada ya kutokea mgomo chuoni hapo leo asubuhi.
Mmoja wa wanafunzi  wa chuki kikuu cha Iringa akitoa malalamiko yake dhidi ya  bodi ya mikopo kwa kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Angeline Mabula leo kuhusu kucheleweshewa  mikopo yao.
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Mabula akizungumza na wanafunzi hao wakati wa mgomo wa wananchuo wa chuo cha RUCU leo
Ulinzi   ulikuwa ni wakutosha chuoni hapo (Picha na Francis Godwin)


Jeshi la polisi mkoani Iringa limelazimika kutumia nguvu kuwatawanya wanafunzi wa chuo kikuu cha Rucu baada ya kutaka kufanya maandamano na kusababisha vurugu chuoni hapo.
Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi ameeleza kuwa wanafunzi hao walitaka kufanya maandamano hayo kwa madai kuwa wamecheleweshewa mikopo yao.
Kamanda amesema kuwa wamewadhibiti  wanachuo hao ili wasitoke nje ya geti la chuo kutokana na kuhofia kuvuruga amani .
Aidha kamanda ameeleza kuwa jeshi la polisi linawashikilia wanafunzi 89 na kusema kuwa kwa yoyote atakayejaribu kuvunja amani ni lazimawatamchukulia hatua kali za kisheria bila kujari chochote.
Hata hivyo wakizungumza wanachuo hao wamesema kuwa kucheleweshwa kwa mikopo hiyo kunachangia maisha yao kuwa magumu.
Wakati huo huo Jeshi la hilo linawashikilia viongozi watatu wa waendesha pikipiki kwa tuhuma za kuwafanyia fujo maafisa watatu wa mamlaka ya usafirishaji wanchi kavu na majini Sumatra.
Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi amesema kuwa maafisa hao wamefanyiwa fujo wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kawaida katika eneo la chuo cha mkwawa manispaa ya Iringa.
Kamanda amesema kuwa jeshi la polisi tayari limeshafungua jalada na watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani muda wowote yatakapoletwa mashtaka.
Aidha kamanda amesema kuwa endapo matukio kama hayo hayata kemewa mapema yatachangia uvunjifu wa amani hivyo amewataka wananchi pamoja na wanahabari kushirikiana kwa pamoja katika kukemea masuala hayo.
Hata hivyo akizungumza afisa mfawidhi wa mamlaka ya usafirishaji wa nchi kavu na majini Sumatra mkoa wa iringa Bartel Patel amekiri kufanyiwa kwa kitendo hicho.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA