Rais wa Burundi
Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza kufungwa kwa mipaka
1 Mwandishi wa BBC huko Bujumbura Kazungu Lozy anasema watu wangali wanasheherekea Rais Nkurunzinza ameingia ndani ya gari lake na kuondoka mjini Dar es Salaam akionesha dalili kuwa yuaelekea BurundiKiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid Niyombare
18:37
Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid
Niyombare ameamrisha wanajeshi kuzuia rais Nkurunzinza kutua Burundi
18:30 Rais Pierre Nkurunziza anatarajiwa kuhutubia taifa baada ya kurejea kutoka Tanzania amesema msemaji wake Willy Nyamitwe.Wananchi waendelea kusheherekea Bujumbura kufuatia tangazo la ''Mapinduzi''
18:25 Generali Niyombareh ametoa amri kwa majeshi kuungana na kulinda viwanja vya ndege kote nchini humo
18:20
Generali aliyeongoza ''Mapinduzi'' leo asubuhi amewataka maafisa wa
jeshi na polisi kufanya kazi kwa pamoja ilikulinda usalama wa nchi hiyo.Rais kikwete alipohutubia waandishi wa habari Dar es Salaam akiandamana na Rais Nkurunzinza
18:15 Viongozi wa kanda ya Afrika wametaka makundi hasimu kutulia na kukubali hali ya kikatiba Kurejea
18:10 Esipisu amesema kuwa rais Uhuru Kenyatta anaunga mkono kurejeshwa kwa utawala wa kikatibaMaafisa wa jeshi la Burundi wakisheherekea Barabarani Bujumbura
18:07 Msemaji wa rais wa Kenya Manoah Esipisu amesema kuwa viongozi wanataka hali ya kawaida irejee huko BurundiRais Uhuru Kenyatta akiwa Tanzania
18:06 Rais wa Tanzania amekashifu ''mapinduzi'' yaliyotoke leo huko Burundi
18:05 Rais amesema hayo katika mkutano wa upatanishi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki
18:01 Ujumbe wa mtandao wa facebook wa urais nchini Burundi umekanusha kutokea kwa ''Mapinduzi''.Raia wakisheherekea ''Mapinduzi''
18:01 Viongozi hao wanakutana dar es salaam kujaribu kutatua mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi
18:01 Rais Jakaya Kikwete amesema hayo katika mkutano wa upatanishi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki
18:00 Rais wa Tanzania amekashifu ''mapinduzi'' yaliyotoke leo huko Burundi
17:55 Msemaji wa rais Nkurunzinza ameiambia BBC kuwa asilimia 95 ya taifa hilo ingali salama na wala hakuna tashwishi.Manuari za kijeshi zingali barabarani mjini Bujumbura
17:50 Manuari zaidi zaonekana barabarani mjini Bujumbura
17:45 Ujumbe wa mtandao wa facebook wa urais nchini Burundi umekanusha kutokea kwa ''Mapinduzi''.
17:30 Msemaji wa rais Nkurunziza,Willy Nyamitwe ameiambia BBC kuwa rais huyo angali madarakani na kuwa hajaondolewa madarakaniRaia wakiwazoma maafisa wapolisi ambao awali walikuwa wakikabiliana nao
17:22 Redio ya taifa ya Burundi inasema kuwa rais Nkurunzinza angali Madarakani na kuwa hakujakuwa na ''mapinduzi''Raia wakikumbatiana katika bustani la uhuru Bujumbura
17:20 Maafisa wa jeshi wanaolinda kituo cha taifa cha redio wamewaonya watangazaji wasitangaze kuwa kuna ''mapinduzi''
17:05
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Ruth Nesoba anasema kuwa waandamanaji
wamefululiza hadi kwenye vituo vya polisi na magereza yaliyokuwa na
mahabusu waliokamata kwa kuandamana na kuwaachilia huruWanajeshi ya Burundi wakijaribu kutuliza hali Bujumbura
17:00 Redio ya taifa inasema kuwa bado rais Nkurunzinza angali madarakani.
16:50 Kituo hicho cha redio cha ''African Public Radio'' kinapeperusha tangazo la kupinduliwa kwa serikali ya rais NkurunzinzaRaia wanasherehekea ''kupinduliwa'' kwa Nkurunzinza
16:40 Redio iliyokuwa imefungwa na serikali ya rais Nkurunzinza kwa kupeperusha habari za maandamano imefunguliwa upya.
16:30 Mwandishi wa BBC Cyriac Muhawenay aliyeko Bujumbura anasema raia wanaonekana kuwa na furaha.
16:20 Picha za raia wakiwa wamekwea vifaru vya kijeshiVifaru vya kijeshi katikati ya mji mkuu Bujumbura
16:08 Watu wanaonekana wakininginia kwenye vifaru vya jeshi
16:05 Afisi ya urais nchini Burundi imetangaza kwenye mtandao wake wa twitter kuwa ''hali ni Shwari''Raia wakishangilia ''mapinduzi''
16:00 Majeshi wameonekana nje ya kambi za kijeshi mjini Bujumbura
15:58 Viongozi wa jeshi wamewaamrisha maafisa wa polisi kuondoka mabarabarani.Raia wakiwa wamekwea vifaru vya kijeshi Bujumbura
15:55
Mwandishi Sonia Rolley, wa Radio France International anasema kuwa
halaiki ya raia wamefika nje ya kituo hicho wakishangilia matukio hayoWaandamanaji Bujumbura
15:50 Waandamanaji wanasemekana kuambatana na wanajeshi kuelekea katikati ya mji mkuu wa Bujumbura
15:45
Rais Pierre Nkurunziza ambaye analaumiwa kugombea urais kwa muhula wa
tatu, anatarajiwa kuhudhuria mkutano huo, kusikiliza hoja za viongozi
wenzake.Waandamanaji Bujumbura
15:40 Mwandishi wa BBC aliyeko Bujumbura Maud Julien anasema kuwa Miili ya watu watatu imeonekane katika barabara za Bujumbura
15:36 Viongozi wote wa kanda ya Afrika Mashariki na kati wako Dar es Salaam kwa mwaliko wa rais Kikwete.Raia wanashangilia mjini Bujumbura
15:35
Rais Nkurunzinza yuko mjini Dar es Salaam Tanzania kuhudhuria mkutano wa
kutafuta suluhu ya mgogoro wa kisasa uliokuwa ukiendelea Burundi.
15:30
Maelfu ya raia wa Burundi waandamana a mabarabarani mjini Bujumbura
wakishangilia tangazo hilo la ''kutomtambua'' rais Nkurunzinza.Maafisa wa jeshi la Burundi wanaonekana wakiweka usalama
15:20
Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari anasema kuwa
Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za
kimataifa.
15:10
Meja Generali Niyombareh amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa
Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza.Maafisa wa polisi wamekuwa wakipambana na waandamanaji wanaopinga hatua ya Rais Nkurunzinza kuwania awamu ya tatu
15:05 Jenerali Niyombareh alikuwa ameandamana na viongozi wengine wa jeshi la Burundi.
15:00 taarifa zaibuka kutoka Burundi kuwa rais Nkurunzinza ameng'olewa'' madarakani.
Ripoti
kutoka Bujumbura zinasema kuwa kamanda mmoja wa kijeshi ametangaza kuwa
hamtambui tena Pierre Nkurunziza kama rais wa BurundiPolisi wameamrishwa kuondoka mabarabarani
Meja
Jenerali Godefroid Niyombareh amewaambia waandishi wa habari mjini
Bujumubura, kuwa kumeundwa kamati maalum ya kuiokoa Burundi
itakayotawala taifa hilo kwa kipindi cha mpwito.
Kulingana na taarifa iliyopeperushwa na redio Isanganiro, serikali ya Nkurunziza imeon'golewa madarakani.Raia wa Bujumbura wakishanilia tangazo la generali Niyombareh
Meja
Generali Niyombareh amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa
Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza.
Jenerali
huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari anasema kuwa Nkurunziza
alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa.Meja
Jenerali Godefroid Niyombareh amewaambia waandishi wa habari mjini
Bujumubura, kuwa kumeundwa kamati maalum ya kuiokoa Burundi
Kwa sasa
rais Nkurunziza yuko nchini Tanzania alipokuwa anatarajiwa kujumuika na
viongozi wa kanda hii ya Afrika Mashriki kutafuta suluhu ya mgogoro wa
Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu.
Jenerali Niyombareh alikuwa ameandamana na viongozi wengine wa jeshi la Burundi.
Tayari wanajeshi wameshika doria nje ya makao makuu ya runinga ya taifa.Meja
Jenerali Godefroid Niyombareh amewaambia waandishi wa habari mjini
Bujumubura, kuwa kumeundwa kamati maalum ya kuiokoa Burundi
Rais Nkurunzinza alikuwa amepuzilia mbali maombi ya kuahirisha uchaguzi huo.
Duru kutoka Burundi zinasema kuwa raia wameshajitokeza mabarabarani wakishangilia kauli hiyo ya ''Mapinduzi''
CHANZO BBC SWAHILI
Comments