SHERIA MPYA YA TAKWIMU KUONGEZA UFANISI WA SHUGHULI ZA KITAFITI NA UPATIKANAJI WA TAKWIMU SAHIHI NCHINI.
Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akitoa ufafanuzi
kwa waandishi wa habari kuhusu ujio wa sheria mpya ya Takwimu ya mwaka
2015 iliyopitishwa na Bunge Mwezi Machi mwaka huu leo jijini Dar es
Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi hiyo Bw.
Morrice Oyuke.
Wadau
mbalimbali na waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi
ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa wakati akitoa ufafanuzi kuhusu
ujio wa sheria mpya ya Takwimu ya mwaka 2015.
………………………………………………………….
Na. Veronica Kazimoto. Dar es salaam.
Ofisi ya
Taifa ya Takwimu imesema kuwa Sheria Mpya ya Takwimu ya mwaka 2015 haina
lengo la kuzuia Taasisi au watu binafsi kufanya tafiti zao hapa nchini
bali inalenga kuweka misingi imara ya shughuli za kitakwimu na tafiti
zenye ulinganifu unaotokana na mfumo rasmi utakaoondoa uwepo wa takwimu
zinazokinzana.
Kauli
hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya
Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa wakati akitoa ufafanuzi kwa waandishi
wa habari kuhusu ujio wa sheria hiyo mpya iliyoridhiwa na Bunge Mwezi
Machi mwaka huu.
Amesema
kuanzishwa kwa sheria hiyo kunalenga kutoa mwongozo kwa Taasisi za
Serikali na Mashirika mbalimbali yanayozalisha takwimu hapa nchini ili
yaweze kuendesha shughuli za ukusanyaji na usambazaji wa takwimu kwa
kuzingatia sheria hiyo mpya na kuwa huru kutoa takwimu sahihi
zinazoendana na uhalisia wa Tanzania.
“Sheria
hii hailengi kuondoa uhuru wa taasisi nyinine za utafiti zilizopo
kisheria kufanya kazi zao, taasisi hizo zitaendelea kuwa huru kufuata
taratibu zao ilimradi hazikiuki sheria hii” Amesisitiza Dkt.Chuwa.
Comments