Uongozi wenye Dira, Ubunifu na Ugunduzi – Uaminifu, Uadilifu na Kujituma – Stadi Bulibuli za Usimamizi na Uzoefu katika Uongozi – Uwazi na Ufanisi – Matokeo Yenye Tija na Ubora wa Hali ya Juu
Prof Dkt Sospeter Muhongo, mwanazuoni maarufu, mwanajiolojia
mbobevu na Mbunge wa Kuteuliwa, amewahi kuwa Waziri wa Wizara ya
Nishati na Madini wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (April 2012-
Januari 2015). Serikali ya Ufaransa ilimtunukia Cheo cha Afisa
Mwenyetunu ya Kitaaluma Iliyotukuka – Ordre des Palmes AcadΓ©miques
(Iliyoanzishwa na Mfalme NapolΓ©on Mwaka 1808) na ni mtu wa kwanza
kupokea Tuzo (Mwaka 2004) inayoheshimika sana kwa Jamii ya
Wanajiolojia wa Afrika ya Prof Robert Shackleton (UK) (Geological
Society of Africa’s prestigious Prof Robert Shackleton Award), kwa ajili ya
utafiti wa kipekee kuhusu Jiolojia ya Afrika ya miamba yenye umri wa
zaidi ya miaka Milioni 500 (Precambrian Geology of Africa).
Kwa kutambua mchango wake mkubwa wa kimataifa katika Sayansi na Ustawi wa Jamii
ulimwenguni, Prof Muhongo amepewa nafasi nyingi zenye kuheshimiwa na wasomi na wataalamu
maarufu Duniani, pamoja na kutambulika kwa ngazi za juu kabisa na Vyama na Taasisi zao za
kitaaluma, kwa mfano: An Honorary Fellow of the Geological Society of London (Ilianzishwa Mwaka
1807), Honorary Fellow of the Geological Society of America (Ilianzishwa Mwaka 1888), an Honorary
Research Fellow of the Chinese Academy of Geological Sciences (Ilianzishwa Mwaka 1956).
Ni Mshiriki wa Ngazi ya Juu (Fellow) wa Akademia ya Sayansi ya Nchi Zinazoendelea (FTWAS),
Mshiriki wa Ngazi ya Juu (Fellow) wa Chama cha Wanajiolojia wa Afrika (FGSAf) , Mshiriki wa Ngazi
ya Juu (Fellow) wa Akademia ya Sayansi ya Afrika (FAAS) na Mshiriki wa Ngazi ya Juu (Fellow) wa
Akademia ya Sayansi ya Tanzania (FTAAS) na nyingine kadhaa. Ni Makamu wa Rais Mstaafu wa Tume
ya Ramani ya Jiolojia ya Dunia (CGMW) na pia Mhariri Mkuu Mstaafu wa Jarida la Afrika la Sayansi za
Miamba na Madini (The Journal of African Earth Sciences, Elsevier). Prof Muhongo ni Mshindi wa
Mwaka 2014 wa Tuzo ya Heshima ya Jamii ya Wanasayansi wa Jiolojia na Uchimbaji Petroli na Gesi
Asilia ya Nigeria (NMGS)/AMNI ya Prof M.O. Oyawaye.
Prof Muhongo aliongoza na kusimamia mabadiliko endelevu ya ubunifu na ugunduzi katika Sekta za
Nishati na Madini nchini mwetu kwa kuingiza sera mpya na kutengeneza nyaraka za kisheria,
ameongeza idadi kwa wingi ya rasilimali watu iliyopata mafunzo mazuri ya kitaaluma katika Tasnia ya
Mafuta na Gesi Asilia. Amesimamia ongezeko la kasi kubwa ya kampeni ya usambazaji umeme
vijijini, na amesimamia usambazaji wa haraka na wa uhakika wa umeme mijini. Amesimamia
punguzo kubwa la gharama za kuunganishiwa umeme vijijini na mijini. Amesimamia ongezeko la
mapato katika Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kutokana na kodi na tozo mbalimbali kwenye madini
yetu. Baadhi ya wachimbaji wadogo wamepatiwa mafunzo na ruzuku ya kuboresha uchimbaji wao.
Tarehe 28.02.2015, Chama cha Wachimbaji Wadogo nchini (FEMATA) kilimteua, kwa kauli moja, Prof
Muhongo kuwa Mshauri Mkuu wao.
Prof Muhongo alisimamia utayarishaji wa mageuzi makubwa kwenye Sekta ya Umeme nchini,
ikiwemo TANESCO, na Juni 2014 Wizara ya Nishati na Madini ilitangaza mipango na miradi
itakayotekelezwa kuhakikisha Taifa linapata umeme mwingi wa kutosha mahitaji yake, umeme
unaopatikana kwa urahisi na kwa uhakika, umeme wa bei nafuu na umeme wa ziada (biashara) kwa
manufaa ya uchumi wetu – Electricity Supply Industry Reform Strategy and Roadmap 2014-2025,
Powering Vision 2025.
2
Prof Muhongo amevutia uwekezaji mpya (kutoka ndani na nje ya nchi) wenye mitaji midogo na
mikubwa kwenye Sekta za Nishati, Madini, Mafuta na Gesi Asilia. Haya yote yamechangia ukuaji
mzuri wa uchumi wetu.
Yeye ni Profesa Kamili (mstaafu) wa Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na Profesa wa
Heshima wa Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini. Ni mjumbe wa bodi kadhaa za
uhariri wa majarida ya sayansi na vijarida vya sayansi, teknolojia na ubunifu. Yeye ni Mhariri
Mwandamizi wa Kitabu cha Mwaka 2009 kiitwacho: Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwa Maendeleo
ya Kiuchumi na Kijamii: Simulizi za Mafanikio kutoka Afrika (“Science, Technology and Innovation for
Socio-Economic Development: Success Stories from Africa”).
Prof Muhongo na watafiti wenzake wamechapisha ramani kwa kuzingatia dhana na maarifa ya kisasa
ya Jiolojia, kama vile: Jiolojia na Mashapo Makubwa ya Madini ya Afrika, Jiolojia na Mashapo ya Vito
vya Thamani vya Afrika Mashariki na Ramani ya Jiolojia na Madini ya Tanzania. Hakuna mikopo au
misaada ya fedha ilitumika kutengeneza ramani hizi. Ramani hizi zinatumika kupanua na kukuza
uwekezaji mpya katika Sekta ya Madini Barani Afrika.
Prof Muhongo alikuwa Rais wa Chama cha Wanajiolojia wa Afrika (1995-2001). Alikuwa Mkurugenzi
Mwanzilishi (2005-2010) wa ICSU Ofisi ya Sayansi ya Kanda ya Afrika, Pretoria, Afrika Kusini. Alikuwa
Mwenyekiti wa Bodi ya UNESCO-IUGS-IGCP Programu ya Kimataifa ya Sayansi ya Jiolojia (2004-
2008), na Mwenyekiti (2007-2010) wa Kamati ya Programu ya Kisayansi (SPC) ya Mwaka wa
Kimataifa wa Sayari ya Dunia uliotangazwa na Umoja wa Mataifa (UN-IYPE). Prof Muhongo aliteuliwa
na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mgombea (2009) wa nafasi ya Mkurugenzi
Mkuu wa UNESCO.
Alikuwa Mwenyekiti (1999-2005) wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Taifa la Madini (STAMICO),
Tanzania; na alikuwa Mkuu wa Idara ya Jiolojia, Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (1997-2000). Prof
Muhongo alikuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi ya Serikali ya Tanzania kuhusu ajali mbaya ya
vifo katika migodi ya Mererani (2002). Prof Muhongo alisimamia kwa umakini mkubwa uboreshaji
wa rasilimali watu, majukumu, miradi na utendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Shirika
la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC).
Prof Muhongo amechapisha zaidi ya makala (publications) 200 za sayansi ya hadhi ya juu zikiwa ni za
kiutafiti zenye kukubaliwa na kurejelewa na watalaamu Duniani kote. Ametoa mihadhara ya
kisayansi zaidi ya 500 akiwa ndiye Mzungumzaji Mkuu (Keynote Speaker) katika Mikutano ya
Kimataifa na Kitaifa. Kwa zaidi ya miongo miwili, Prof. Muhongo ameandaa vikao zaidi ya 100 vya
mikutano ya vikundi vya wataalamu wa Kitaifa na Kimataifa vya sera, teknolojia na sayansi za nishati,
miamba, madini, maji, tabianchi na mazingira. Amekuwa Mwandishi Mkuu wa mikutano ya sera za
sayansi ikiwa ni pamoja na “Sayansi na Afrika” ambayo inadhaminiwa na Kamisheni ya Umoja wa
Mataifa ya Uchumi kwa Afrika (UNECA), Kamisheni ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika (AU) na
washirika wake.
Prof. Muhongo amepata tuzo mbalimbali za kiuanazuoni na kitaalamu, ametambuliwa na kupata
hibafedha kwa kazi mbalimbali za kitaaluma pamoja na kutunukiwa fedha za utafiti. Ameshirikiana
na wanasayansi mabingwa wa Mabara yote kwenye tafiti za kisayansi. Alisomea Jiolojia katika Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam (Tanzania) na Gӧttingen (Ujerumani). Alihitimu na kutunukiwa shahada ya
Dr.rer.nat. kutoka Technical University of Berlin, Ujerumani. Prof. Muhongo anaongea, na kuandika
kwa ufasaha na umahiri mkubwa Kiswahili, Kiingereza na Kijerumani, na kwa wastani kwa lugha ya
Kifaransa.
Comments