UP TODATE ZA HALI TETE NCHINIBURUNDI

Mnamo 13 mwezi May jenerali mmoja wa jeshi alitangaza katika redio ya taifa kwamba rais wa Burundi amepinduliwa na kwamba serikali ya mpito itabuniwa.Lakini msemaji wa rais alikana habari hizo akidai kuwa kulikuwa na usaidizi mdogo katika jeshi kwa mapinduzi kutendeka.Rais Nkurunziza alidaiwa kurudi nchini Burundi kutoka Tanzania ,lakini imethibitishwa kuwa leo, alishindwa kufanya hivyo na kwamba yungali nchini Tanzania.


18.05pm-Wanajeshi watiifu

Makundi hasimu ya jeshi la Burundi yamekuwa yakipambana kukidhibiti chombo cha kitaifa cha habari RTBN ambacho kilizimwa kwa mda .Duru zimearifu kuwa kituo hicho cha habari kiko chini ya udhibiti wa vikosi vinavyomtii rais Pierre Nkurunziza.

17.53pm-Viongozi wajadili Burundi
Baraza la usalama la umoja wa Afrika laijadili Burundi kwa sasa
Baraza la usalama la umoja wa Afrika limetuma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter likisema kuwa wanachama wa baraza hilo kwa sasa wanaijadili.


17.00pm-Wanajeshi wapiga doria
Maafisa wa polisi wapiga doria Burundi
Maafisa wa polisi waliojihami katika mji mkuu wa Burundi,Bujumbura wanaonekana wakilinda vizuizi vya barabarani leo


16.50pm-Mkutano kuhusu Burundi waendelea.
Mkutano wa baraza la usalama la Umoja wa Afrika
Baraza la usalama la umoja wa Afrika kwa sasa linaijadili Burundi.
tweets: "Chini ya Uongozi wa balozi Amina Diallo wa Niger,ni mkutano wa 507.Baraza hilo linaangazia hali ilivyo Burundi


16.10pm-RNTB yarudisha matangazo
Kituo cha redio cha Burundi RNTB kimerudi hewani,chini ya wanajeshi walio watiifu kwa rais Pierre Nkurunziza kulingana na duru kutoka kwa wanajeshi.Tumethibitisha kuwa kimeanza kurusha tena matangazo.


15.50pm-Nkurunziza asema yuko tayari kusamehe
Shirika la habari la Reuters limenukuu baadhi ya mahojiano yaliofanywa na rais Nkurunziza na kituo cha habari cha RTNB mapema leo.
''Ninalishtumu kundi lililopanga mapinduzi'',alinukuliwa akisema.
''Nwashkuru wanajeshi wanaorudisha hali ya kawaida na namsamehe mwanajeshi yoyote ambaye yuko tayari kusalimu amri''.
Lakini baada ya mahojiano hayo kulikuwa na vita karibu na kituo hicho cha habari ambacho kwa sasa kimezimwa.
15.47pm-Ramani ya Burundi
Ramani ya taifa la Burundi.


15.45pm-Mji wa Bujumbura



15.30pm-Vyombo vya habari vyazimwa
Kituo cha habari cha Burundi Isanganiro kimesema kuwa kimefungwa na vituo vyengine vya kibinafsi .Kituo hicho ni miongoni mwa vile vilivyotangaza mapinduzi siku ya jumatano.


15.17pm-Kituo cha habari
Kituo cha habari cha Redio ya RTNB kimezimwa kufuatia mapigano makali karibu na afisi zake mjini Bujumbura.


15.01pm:Rais wa Burundi Ahojiwa

Kituo cha habari cha Burundi RTBN kimemhoji rais Pierre Nkurunziza kwa simu mwendo wa saa sita.Vita vimezuka karibu na afisi za kituo hicho cha habari.Jenerali anayeunga mkono jaribio hilo la mapinduzi amekiambia chombo cha habari cha AFP kwamba vitengo vinavyopigana kumpindua vimepata agizo la kukiteka kituo hicho habari cha RTNB kwa kuwa wana uwezo.


14.30pm:Makundi ya vijana waliojihami
Kuna madai kwamba kundi la vijana linalunga mkono serikali limeshambulia kituo kimoja cha habari cha kibinafsi mjini Bujumbura.KUndi hilo linalojulikana kama Imbonerakure,baadhi ya watu wanaamini kwamba vijana hao wanatumiwa kama wapiganaji na kwamba huenda wamepewa silaha ili kuwatishia raia kabla ya uchaguzi.


13.45pm-Hali ni tete Burundi
Hali bado ni tete nchini Burundi siku moja tu baada ya jenerali mmoja wa jeshi kujaribu kutekeleza mapinduzi .Barabara nyingi zimeendelea kuwa bila watu kwa kipindi kirefu cha alfajiri huku wengi wakisalia ndani ya majumba yao wakihofia usalama kulingana na mwanahabari wetu Ruth Nesoba.


13:30pm-Ukabila

Tofauti zilizopo katika jeshi la Burundi kufuatia jaribio la mapinduzi hazionekani kuwa katika misingi ya kikabila ,mkuu wa majeshi ambaye ni mtiifu kwa rais Nkurunziza pamoja na jenerali wa majeshi aliyetangaza mapinduzi hayo ni wa kabila la Hutu.Makundi hayo yanaonekana kugawanyika kati ya wale wanaoamini rais Nkurunziza alikiuka makubaliano ya amani yaliomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa kutaka kuongoza kwa muhula wa tatu na wale wanaosalia kuwa watiifu kwake


12:05pm-Wanajeshi watiifu
Afisa mmoja wa kijeshi ameiambia BBC Afrique kwamba wanajeshi watiifu nchini Burundi wanadhibiti mji wa Bujumbura ,uwanja wa ndege,makao ya rais pamoja na vituo vya redio na runinga.


12:00pm-Milio ya Risasi

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU