Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Bernad Membe amefungua
Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi uliolenga kujadili masuala
mbalimbali ikiwemo urejeshaji wa wafanyakazi wa wizara yake walioko nje
ya nchi .
Hayo
yasemwa leo na Waziri Membe alipokuwa akifungua mkutano huo ulihusisha
wafanyakazi wa Wizara pamoja viongozi wa TUGHE,kwa lengo la kuweka
mikakati madhubuti ya kuboresha mazingira ya kazi kwa kila mtumishi wa
Wizara hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
"Tunatarajia
kupata bilioni 300 zitakazotusaidia kuwarudisha nchini wafanyakazi wote
45 wa Wizara waliomaliza mikataba yao kazi huko nje ndani ya miezi
mitatu, ilikuwapa nafasi wafanyakazi wengine nao kwenda kutekeleza
shughuli walizokuwa wakizifanya wa kwani hii inasaidia kuwapa fursa
mkubwa kila mtumishi wa kupata ujuzi mkubwa kutoka kwa watu
wengine",alisema Mhe.Membe.
Naye
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Diaspora Bibi. Rose Jairo wa alimpongeza
Waziri Membe kwa juhudi zake mbalimbali alizozifanya katika Wizara hiyo
ikiwemo kuanzisha kitengo cha Diaspora pamoja kukisimamia kwa madhubuti
katika kuhakikisha kinafanya kazi kwa uhakika na kuleta tija kwa
Serikali.
"Mhe.Waziri
tunakupongeza kwa jitihada zako ulizozifanya katika Wizara yetu pia
umekuwa kiongozi mwenye kujali maslahi ya kila mtumishi na pia kuna
mambo mengi mazuri umeyafanya ikiwemo kuboresha maslahi ya wafanyakazi
kuwapa nafasi za kwenda kusoma nje na kuwatafutia nafasi za mafunzo
nje",alisema Bibi Jairo.
Mbali na
hayo naye Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam Bw.Gaudensi Kidingo
aliipongeza wizara ya mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa kwa
kuzingatia ratiba na kuweza kufanya vikao vyote vya wafanyakazi,pia
ameiomba wizara kujaribu kuzingatia muda wa kufanya mkutano wa Baraza la
wafanyakazi ili TUGHE wawezekupata muda mzuri wa kushauri menejimenti.(V.S)
Comments