Askari watoto wasajiliwa Islamic State

Picha za video katika simu ya mkononi ambazo BBC imezipata zinaonekana kuwaonyesha wapiganaji wa Islamic State wakimtesa mvulana wa Syria mwenye umri wa miaka 14.
Picha hiyo ambayo ilipigwa na mpiganaji aliyeasi kutoka kikundi hicho, inaonyesha mvulana huyo akipigwa wakati amefujngwa mikono yake.
Umoja wa Mataifa umeishutumu IS na makundi mengine yenye silaha nchini Syria na Iraq kwa kuwatesa na kuwaua watoto.
Watoto walisajiliwa, kufunzwa na kutumiwa katika uwanja wa vita.
Kijana mwingine ameiambia BBC namna alivyopigana na kuua kwa ajili ya kikundi cha al-Nusra Front chenye uhusiano na al-Qaeda. Wakati huo alikuwa na umri wa miaka 15 tu na wakati huo alipojiunga na IS alimkuta kijana wa miaka 13 akifundishwa itikadi kali ya kidini.
Mvulana wa Syria akiadhibiwa na mpiganaji wa IS
Picha ya simu ya mkononi inamwonyesha Ahmed akiwa amening'inizwa mguu juu.
Amefungwa kitambaa usoni, na wanaume wawili wakiwa wameficha sura zao, wakiwa wamevaa nguo nyeusi kutoka juu hadi chini ya vidole vya miguu. Mmoja ana kifu na bastola na mwingine ana hangaika chumbani akiwana bunduki aina ya AK-47.
Ndani ya maeneo waliyojitangzia kuyatawala, Islamic State imeondoa mfumo wa elimu ya kawaida na badala yake kuanzisha shule za mtindo wa kijeshi ambazo zinawafundisha watoto iutikadi kali ya kidini na kuwafundisha kuua.
Islamic State wamekuwa wakiua nchini Syria na Iaraq, lakini madhara yake yataonekana zaidi baadaye.
Huu ni ufisadi wa karne. Watoto wa IS watakua kuwa watu wazima wakiwa wamefundishwa kuua na kujaa chuki na watazisumbua Syria na Iraq kwa miaka mingi ijayo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI