London,Uingereza,
Mkuu
wa usalama wa taifa wa nchi ya Rwanda Major Gen.Emanuel Karenzi Karake
amekamatwa na wanausalama katika uwanja wa ndege wa Heathrow nchini
Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita,kwa kutuhuma za mauaji ya kivita
mwaka 1994 na baada ya mwaka huo pia.
Major Gen.Karenzi Karake aliwekwa kizuwizini na baadaye kufikishwa katika mahakama ya Westminister,amri ya kukamatwa kwa
mkuu huyo wa idara ya ujasusi (NISS) ya Rwanda kunatokana na ombi la
mahakama ya nchi ya Spain ambayo imeorodhesha watu wapatao 40 kuhusika
na makosa ya kivita nchini Rwanda ,mashataka yalifunguliwa 2008 kufuatia
uchunguzi uliofanywa na kikosi cha mahaka ya spain kinachoongozwa na
Andreu Melles .
Mkurugenzi
mkuu huyo wa usalama wa taifa wa Rwanda Bw.Karenzi Karake mwenye umri
wa miaka 54 bado yupo kiziwizini na anatagemea kupandishwa Kizimbani
tena siku ya Alhamisi.
Comments